NENO “KAMA”LACHANGANYA.
Neno
“kama” kweli gumu,kulitumia vigumu,
Kama
wasoma isimu,tupunguzie ugumu,
Lugha
si mwanaharamu,nayo inayo rasimu,
Neno “kama”lachanganya,jamani
tuwe makini.
Mimi
“kama’ ni mwalimu,wiki hii niko
zamu,
Nikikukuta
sehemu,usije kunilaumu,
Mwalimu
ulihitimu,”kama”hapo si sehemu,
Neno “kama”lachanganya,jamani
tuwe makini
Mheshimiwa
hakimu,kazi yako kweli ngumu,
Unaposoma
hukumu,roho kweli iwe ngumu,
Na
mimi “kama” hakimu,mvua sita kazi
ngumu,
Neno “kama”lachanganya,jamani
tuwe makini
Mimi
“kama”mhudumu,faili zamu kwa zamu,
Wote
muwe na nidhamu,nisjie panda wazimu,
Kazi
yangu mfahamu,ni ngumu msilaumu,
Neno “kama”lachanganya,jamani
tuwe makini
N
a mimi “kama”Adamu,nimemzaa Swaumu,
Mtoto
wangu wa damu,Mola amenirehemu,
Nitampenda
dawamu,kama mwana wa Kikwemu,
Neno
“kama”lachanganya,jamani tuwe makini
Mbunge
wetu udumu,hii ni yako awamu,
Watu
wako tuna hamu,tatua kero kwa zamu,
Na
mimi “kama”mwalimu,kusema siishi
hamu,
Neno “kama” kwa hakika,hapo ni mahala pake.
Viongozi
silaumu,neon hilo kwenu gumu,
Mwatushushia
“mabomu”,najua hamfahamu,
Mbona
mkijaza fomu,huwa mnalifahamu,
Neno “kama”lachanganya,jamani
tuwe makini
Naweka
chini kalamu,neno “kama”lifahamu,
Sio
kuwa nashutumu,neno “kama”sina hamu,
Ninawaomba
walimu ,lirudisheni utamu,
Neno
“kama”lachanganya,jamani tuwe makini
Konisaga
Mwafongo
Simu:0717 24 88 28