wengi twapenda karamu,twazisubiri kwa hamu,
kama hili hufahamu,jibu utapata humu,
utavipata vitamu,kamwe hutapata sumu,
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
nilichukua kalamu,kueleza umuhimu,
ninataka kufahamu,japo katika awamu,
karamu sio swaumu,kupata si jambo gumu,.
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
karamu nyingi fahamu,zaweza kuleta pumu,
jinsi tunavyozifomu,nyingizo sio muhimu
kuzijua nina hamu,moyo pate tabasamu
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
mimi ninavyofahamu,karamu si marhamu,
imeshaniisha hamu,nitamwuliza mwalimu,
vipi hizo zinadumu,tena daima dawamu,
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
unajilipua bomu,tena huku wafahamu,
hiyo kwako ni karamu,kweli huna ufahamu,
ulitumia vidumu,kuliunda hilo bomu,
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
wanipatia salamu,moyoni huna fahamu,
waanza kumwaga sumu,ofisini nisidumu,
umekuwa ni hasimu,kama unavuta'ndumu'
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
ndoa yangu haidumu,unajifanya hakimu,
asubuhi wajihimu,unaleta uhasimu,
kwetu wewe si Rahimu,ndoa yetu itadumu,
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
ninapenda ufahamu,sitaki ugomvi humu,
wapi ulikohitimu,feki wako ualimu,
unatushusha stimu,nenda zako jehanamu
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
No comments:
Post a Comment