keki sana twaipenda,sote twaipigania,
mdomoni twaisonda,na macho tunatumbua,
wengineo wanainda,yote wajichukulia,
keki kaleta mgeni,wenyeji twagombania.
alipofika mgeni,keki ilikuwa yake,
nasi tukaitamani,japo ilikuwa kwake,
iko siku tutawini,bila tumia makeke,
keki kaleta mgeni,wenyeji twagombania.
mgeni akaondoka,keki akatuachia,
sasa tunafurahika,keki twaifurahia,
vipande vikidondoka,vyote kujiokotea,
keki kaleta mgeni,wenyeji twagombania.
keki ilikuwa moja,sasa tunaigawana
tulikuwa ni wamoja,sasa tunafarakana
imeuvunja umoja,mapanga tunakatana,
keki kaleta mgeni,wenyeji twagombania.
keki yao sio safi,kama zetu za asili,
keki yao kama fifi,katu hutamani huli,
ni nyepesi kama sufi,keki hiyo mimi sili
keki kaleta mgeni,wenyeji twagombania.
keki imeleta vita,wote imetugawanya,
kusema mi sitasita,nimepata huu mwanya,
beti zikifika sita,ujumbe waweza penya,
keki kaleta mgeni,wenyeji twagombania.
amerudi kwa ujanja,na keki nyingine tena,
udugu tumeuvunja,kutwa kucha twagombana,
keki hizo tumeonja,sasa tunafarakana,
keki kaleta mgeni,wenyeji twagombania.
keki zao kumbe chungu,tulidhania ni tamu,
nasema haki ya Mungu,imeshaniisha hamu,
sitaki nyumbani kwangu,keki hizo kweli ngumu,
keki kaleta mgeni,wenyeji twagombania
.
kila mtu atamani,keki achukue yote,
utu hauna thamani,wokovu tukaupate,
keki za kihayawani,hadi vichwa watukate,
keki kaleta mgeni,wenyeji twagombania.
chukueni keki zenu,kwanza zaleta majanga,
hebu rudisheni kwenu,tumevichoka visanga,
keki zenu ni za kwenu,sasa tumepata mwanga,
keki kaleta mgeni,wenyeji twagombania.
Thursday, October 6, 2011
Thursday, September 29, 2011
PETE
pete kitu cha ajabu,kwangu inaleta adha,
zipo pete za dhahabu,na pia zile za fedha,
avaa kaka Twalibu,na pia dada Faidha,
nani aivae pete,na nani asiivae?.
mimi nilifikiria,pete ni za wana ndoa,
kidole cha kuvalia,cha pete sote twakijua,
lakini ninashangaa,sipo wanapovalia,
hakika sijaelewa,nini maana ya pete.
kama ni ya wana ndoa,mbona wengi wanavua,
nini wanadhamiria,vidoleni waitoa,
jibu kweli sijajua,wao watatupatia,
jamani sijaelewa,wapi pa kuvaa pete.
kama ni uaminifu,mbona wengi wazinifu,
wajitia watiifu,na mioyo mikunjufu,
tabia zao zakifu,zatia kichefuchefu,
hizo pete mnavaa,sijui maana yake.
hata kwenye maandiko,kule kwenye biblia,
ukienda soma huko,mengi utajipatia,
utapata muamko,maana utaijua,
yule mwana mpotevu,ndiye alivishwa pete.
ndoa sio upotevu,sisi tuvae za nini,
kama ni uvumilivu,hilo latoka moyoni,
yataka ustamilivu,uweze kuibaini,
pete nivae ya nini,sijui maana yake.
hata wanaozivaa,mambo yao ya kihuni,
wale wanaozivua,tabia utabaini,
bora asiyeivaa,akamtii Manani,
ukweli hutobaini,kuhusu pete ya ndoa.
wengi wanaziabudu,'mipete'vidole vyote,
haya mambo ya ajabu,utayaona popote,
'mipete'sio thawabu,hilo jambo kweli tete,
'mipete' vidole vyote,inaashiria nini?
kwa maumbo zipo nyingi,nyingine zinachukiza,
masonara wako wengi,urembo kuziongeza,
maswali zazua mengi,vigumu kujieleza,
pete mfano wa chura,mnazivaa za nini?
angalia vidoleni,'mipete ni ya ajabu,
mna nini fikrani,kwangu sioni sababu,
kwangu sawa na majini,sitaweza zijaribu,
pete ya ndoa unayo,nyingine za kazi gani?
nyingine zatoka wapi,maumbo siyo bayana,
hata kama mmekopi,za ndoa zitofanana,
hivi hamziogopi,enyi wana wa Rabana,
vaeni hiyo 'mipete',mseme maana yake.
hayo ni mawazo yangu,japo yatia uchungu,
pete sitovaa kwangu,wala familia yangu,
hata mnifunge pingu,sitaki kidole changu
Yule mwana mpotevu,ndiye alivikwa pete.
zipo pete za dhahabu,na pia zile za fedha,
avaa kaka Twalibu,na pia dada Faidha,
nani aivae pete,na nani asiivae?.
mimi nilifikiria,pete ni za wana ndoa,
kidole cha kuvalia,cha pete sote twakijua,
lakini ninashangaa,sipo wanapovalia,
hakika sijaelewa,nini maana ya pete.
kama ni ya wana ndoa,mbona wengi wanavua,
nini wanadhamiria,vidoleni waitoa,
jibu kweli sijajua,wao watatupatia,
jamani sijaelewa,wapi pa kuvaa pete.
kama ni uaminifu,mbona wengi wazinifu,
wajitia watiifu,na mioyo mikunjufu,
tabia zao zakifu,zatia kichefuchefu,
hizo pete mnavaa,sijui maana yake.
hata kwenye maandiko,kule kwenye biblia,
ukienda soma huko,mengi utajipatia,
utapata muamko,maana utaijua,
yule mwana mpotevu,ndiye alivishwa pete.
ndoa sio upotevu,sisi tuvae za nini,
kama ni uvumilivu,hilo latoka moyoni,
yataka ustamilivu,uweze kuibaini,
pete nivae ya nini,sijui maana yake.
hata wanaozivaa,mambo yao ya kihuni,
wale wanaozivua,tabia utabaini,
bora asiyeivaa,akamtii Manani,
ukweli hutobaini,kuhusu pete ya ndoa.
wengi wanaziabudu,'mipete'vidole vyote,
haya mambo ya ajabu,utayaona popote,
'mipete'sio thawabu,hilo jambo kweli tete,
'mipete' vidole vyote,inaashiria nini?
kwa maumbo zipo nyingi,nyingine zinachukiza,
masonara wako wengi,urembo kuziongeza,
maswali zazua mengi,vigumu kujieleza,
pete mfano wa chura,mnazivaa za nini?
angalia vidoleni,'mipete ni ya ajabu,
mna nini fikrani,kwangu sioni sababu,
kwangu sawa na majini,sitaweza zijaribu,
pete ya ndoa unayo,nyingine za kazi gani?
nyingine zatoka wapi,maumbo siyo bayana,
hata kama mmekopi,za ndoa zitofanana,
hivi hamziogopi,enyi wana wa Rabana,
vaeni hiyo 'mipete',mseme maana yake.
hayo ni mawazo yangu,japo yatia uchungu,
pete sitovaa kwangu,wala familia yangu,
hata mnifunge pingu,sitaki kidole changu
Yule mwana mpotevu,ndiye alivikwa pete.
Wednesday, September 21, 2011
HONGERA NYASA HONGERA
gazeti nyasa hongera,nyanda za juu kusini,
mambo yaliyotukera sasa,wazi gazetini,
sasa simama imara,upafike kileleni
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
zamani tilipunjika,mwanya finyu tulipewa,
mambo mengi kufichika,wengi hatukuelewa,
sasa yaanza fichuka,mengi yatakuwa sawa,
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
kupata gazeti letu,hakika,tunashukuru,
tutaona mambo yetu,kweli huu ni uhuru,
hata vijijini mwetu,tumeshapata uhuru,
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
makala za kuvutia,'kama ninasema hivi'
zote mnatupatia,hakika ninyi wajuvi,
mashairi yavutia,kama mahiri wavuvi,
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
habari za vijijini,sasa tunajipatia,
tulihamia mijini,riziki jitafutia,
sasa tunayabaini,maendeleo sawia.
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
limeshafika Mshewe,kwake mzee Mwangoka,
liliwatia kiwewe,moyoni kufarijika,
hebu jiulize wewe,mangapi ulipunjika,
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
kaulize Ibungila,kama hawajaliona,
hata ufike Lumbila na majirani Kagwina,
kwake kaka mwasubila,nyasa kwake ajivuna,
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
limefika hata Mbozi,kwake Richadi Ayao,
ameweza nipa dozi,ushauri wa kikwao,
nami natoa pongezi,nyasa limefika kwao,
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
hongereni,waandishi,pia nanyi wahariri,
kujifunza na kuishi,kzai yenu ni mahiri,
msiandike uzushi mtapata soko zuri,
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
mambo yaliyotukera sasa,wazi gazetini,
sasa simama imara,upafike kileleni
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
zamani tilipunjika,mwanya finyu tulipewa,
mambo mengi kufichika,wengi hatukuelewa,
sasa yaanza fichuka,mengi yatakuwa sawa,
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
kupata gazeti letu,hakika,tunashukuru,
tutaona mambo yetu,kweli huu ni uhuru,
hata vijijini mwetu,tumeshapata uhuru,
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
makala za kuvutia,'kama ninasema hivi'
zote mnatupatia,hakika ninyi wajuvi,
mashairi yavutia,kama mahiri wavuvi,
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
habari za vijijini,sasa tunajipatia,
tulihamia mijini,riziki jitafutia,
sasa tunayabaini,maendeleo sawia.
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
limeshafika Mshewe,kwake mzee Mwangoka,
liliwatia kiwewe,moyoni kufarijika,
hebu jiulize wewe,mangapi ulipunjika,
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
kaulize Ibungila,kama hawajaliona,
hata ufike Lumbila na majirani Kagwina,
kwake kaka mwasubila,nyasa kwake ajivuna,
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
limefika hata Mbozi,kwake Richadi Ayao,
ameweza nipa dozi,ushauri wa kikwao,
nami natoa pongezi,nyasa limefika kwao,
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
hongereni,waandishi,pia nanyi wahariri,
kujifunza na kuishi,kzai yenu ni mahiri,
msiandike uzushi mtapata soko zuri,
hongera nyasa hongera,umeleta ukombozi
Tuesday, September 20, 2011
HONGERA NYASA HONGERA
gazeti nysa hongera,nyanda za juu kusini,
mambo yaliyotukera,sasa wazi gazetini
sasa simama imara,upafike kileleni
hongera nyasa hongera umeleta ukombozi
zamani tulipunjika,mwanya finyu tulipewa,
mambo mengi kufichika,wengi hatukuelewa,
sasa yaanza fichuka,mengi yatakuwa sawa
mambo yaliyotukera,sasa wazi gazetini
sasa simama imara,upafike kileleni
hongera nyasa hongera umeleta ukombozi
zamani tulipunjika,mwanya finyu tulipewa,
mambo mengi kufichika,wengi hatukuelewa,
sasa yaanza fichuka,mengi yatakuwa sawa
NDUGU ZANGU MKO WAPI?
kupitia shairini,leo ninatoa zito,
lilokaa akilini,linanitia majuto,
jibu sijalibaini,moyo upate fukuto,
ndugu zangu mko wapi mbona barua sipati?
nikianza na walimu,shule msingi zamani,
walikuwa wakarimu,na roho zenye imani,
kunishikisha kalamu,kunitoa ujingani
ndugu zangu mko wapi mbona barua sipati?
Ndekwa ndiye wa awali,la kwanza alinifunza,
mwalimu Nzogya la pili,tebo ndiye alianza,
naye mama Mtawali,kingereza kunifunza,
ndugu zangu mko wapi mbona barua sipati?
sisahau marafiki,waliokuwa mahiri,
hakujua unafiki,Huseni Juma Omari,
Gene mtoto wa Laki,Mbeya kwenu nafikiri
ndugu zangu mko wapi mbona barua sipati?
Hezroni wa Ruyange,ukweli ulithamini,
kama safari nipange,nije kwako natamani,
hata kama ni Rulenge,nauli nitaiwini
ndugu zangu mko wapi mbona barua sipati?
moyoni nina shauku,nimuone Kachuchuru,
hata kama ni usiku,hakuutoa udhuru,
alikesha kila siku,kusikiza misururu,
ndugu zangu mko wapi mbona barua sipati?
siwezi kutaja wote,anuani yangu chini,
nitasafiri kokote,nikipata anuani,
maisha yapo popote,hapahapa duniani
ndugu zangu mko wapi mbona barua sipati?
Konisaga Mwafongo
0717248828;konisaga@yahoo.com
lilokaa akilini,linanitia majuto,
jibu sijalibaini,moyo upate fukuto,
ndugu zangu mko wapi mbona barua sipati?
nikianza na walimu,shule msingi zamani,
walikuwa wakarimu,na roho zenye imani,
kunishikisha kalamu,kunitoa ujingani
ndugu zangu mko wapi mbona barua sipati?
Ndekwa ndiye wa awali,la kwanza alinifunza,
mwalimu Nzogya la pili,tebo ndiye alianza,
naye mama Mtawali,kingereza kunifunza,
ndugu zangu mko wapi mbona barua sipati?
sisahau marafiki,waliokuwa mahiri,
hakujua unafiki,Huseni Juma Omari,
Gene mtoto wa Laki,Mbeya kwenu nafikiri
ndugu zangu mko wapi mbona barua sipati?
Hezroni wa Ruyange,ukweli ulithamini,
kama safari nipange,nije kwako natamani,
hata kama ni Rulenge,nauli nitaiwini
ndugu zangu mko wapi mbona barua sipati?
moyoni nina shauku,nimuone Kachuchuru,
hata kama ni usiku,hakuutoa udhuru,
alikesha kila siku,kusikiza misururu,
ndugu zangu mko wapi mbona barua sipati?
siwezi kutaja wote,anuani yangu chini,
nitasafiri kokote,nikipata anuani,
maisha yapo popote,hapahapa duniani
ndugu zangu mko wapi mbona barua sipati?
Konisaga Mwafongo
0717248828;konisaga@yahoo.com
ASHA
nimemuona mtoto,kwa jina aitwa Asha,
siyasemi kwa mkato,hakika ninakupasha,
mapigo yapamba moto,lini nitawasilisha,
Jinsi alivyo mzuri,mfanowe sijaona.
kila akitabasamu,macho yake ya bashasha,
katu haiishi hamu,kumtazama si chosha,
kwa kutumia kalamu,sifa zake nitarusha,
hakika ni mtulivu,mtoto aitwa Asha.
Asha ulivyoumbika nani asiyekubali,
mwili ulivyopangika,kila nguo yakubali
wanaume twageuka Mola alivyokujali
watu wote tunawaza nani tampata Asha.
pale ukitabasamu,mwiliwaishiwa nguvu,
nabaki kama sanamu,moyoni ninalo kovu,
pokea japo salamu,unitoe maumivu
asha ninavyokupenda,moyoni hilo wajua
wengi wanakusumbua,kila siku wakufata,
hilo ninalitambua.wote wacheza karata,
kwani ushaangalia,nani kiu atakata,
kukwambia nakwambia,moyo kwako umetua.
pale unapoongea,waongea kwa upole,
nataka kusogelea,nishike japo vidole,
busu nipate tupia,likuchome kama mwale,
kama neno nakupenda,hilo ulishazoea.
mwendo wako taratibu,sana unakupendeza,
wajivuta kwa adabu,nani atayekubeza,
mimi naona sababu sasa nakubembeleza
beti hizo kazi kwako,naomba tuwe pamoja
tena naiangalia,ngozi yako iking'ara,
jinsi ilivyotulia,haina hata harara,
kweli nakusimulia kwa upole si papara,
hakika ninakupenda lugha umeizoea
ngozi yako ni nyororo,laini kama hariri,
sijaona mgogoro,naipenda kwa hiyari,
hutaona hata Moro,nenda hata Ikwiriri,
ngozi bila vipodozi hakika unapendeza.
sauti yako makini,nyoka atoka pangoni,
nimepima kwa makini tafakuri akilini,
nikitazama usoni,ninakupenda mwandani,
wazo najua unalo ni lipi linakutesa
sasa naomba wasaa,baada ya kazi yako,
ninataka nikwambie likae moyoni mwako,
uzito kulipatia,nipate kuwa mwenzako
nini kilichobakia,nimeweka yote wazi,
tukiwa wote nyumbani,nyumba utapendezesha,
utapokuwa jikoni,chakula kuharakisha,
ukifika sebuleni,karibisho kwa bashasha,
wewe ua la nyumbani,karibu nyumbani kwangu
ua nitaweka wapi,sitaliweka juani,
ua sio kama pipi,zinazouzwa dukani,
ua hilo kwa kifupi si kuweka barazani,
ua ninaloongea,hakika ni wewe Asha.
wimbo gani nikwimbie,yote yamejieleza,
lugha gani nikwambie,upate jipeleleza,
shairi nikutungie lipate kukuliwaza,
vyote unavielewa,jibulo litanipoza
sasa chukua kalamu,jaribu andika kitu,
hata kama kwa awamu,si sawa kuacha katu,
kwa wako utaalamu,utaupenya msitu,
mapenzi sawa msitu,kamanda utaupenya
kama sio kwa shairi,tumia japo kauli,
moyoni itoe siri,iweke kwangu mahali,
jibu nishalikariri,nitoe kwenye muhali
nipe japo taabasamu,liwe ndio jibu lako
mashairi yapo mengi siwezi kuyamaliza
sifa zako zipo nyingi,ngapi nitakueleza,
na vikwazo vipo vingi,najua hutoteleza
gari langu liko wazi na abiiria ni wewe.
sasa ninatua hapa,kuandika kwangu jadi,
kama ni nguvu za papa,karata lasti kadi,
naishia hapahapa,kwako naipiga hodi
hodi nilishaipiga nasubiri kuingia.
siyasemi kwa mkato,hakika ninakupasha,
mapigo yapamba moto,lini nitawasilisha,
Jinsi alivyo mzuri,mfanowe sijaona.
kila akitabasamu,macho yake ya bashasha,
katu haiishi hamu,kumtazama si chosha,
kwa kutumia kalamu,sifa zake nitarusha,
hakika ni mtulivu,mtoto aitwa Asha.
Asha ulivyoumbika nani asiyekubali,
mwili ulivyopangika,kila nguo yakubali
wanaume twageuka Mola alivyokujali
watu wote tunawaza nani tampata Asha.
pale ukitabasamu,mwiliwaishiwa nguvu,
nabaki kama sanamu,moyoni ninalo kovu,
pokea japo salamu,unitoe maumivu
asha ninavyokupenda,moyoni hilo wajua
wengi wanakusumbua,kila siku wakufata,
hilo ninalitambua.wote wacheza karata,
kwani ushaangalia,nani kiu atakata,
kukwambia nakwambia,moyo kwako umetua.
pale unapoongea,waongea kwa upole,
nataka kusogelea,nishike japo vidole,
busu nipate tupia,likuchome kama mwale,
kama neno nakupenda,hilo ulishazoea.
mwendo wako taratibu,sana unakupendeza,
wajivuta kwa adabu,nani atayekubeza,
mimi naona sababu sasa nakubembeleza
beti hizo kazi kwako,naomba tuwe pamoja
tena naiangalia,ngozi yako iking'ara,
jinsi ilivyotulia,haina hata harara,
kweli nakusimulia kwa upole si papara,
hakika ninakupenda lugha umeizoea
ngozi yako ni nyororo,laini kama hariri,
sijaona mgogoro,naipenda kwa hiyari,
hutaona hata Moro,nenda hata Ikwiriri,
ngozi bila vipodozi hakika unapendeza.
sauti yako makini,nyoka atoka pangoni,
nimepima kwa makini tafakuri akilini,
nikitazama usoni,ninakupenda mwandani,
wazo najua unalo ni lipi linakutesa
sasa naomba wasaa,baada ya kazi yako,
ninataka nikwambie likae moyoni mwako,
uzito kulipatia,nipate kuwa mwenzako
nini kilichobakia,nimeweka yote wazi,
tukiwa wote nyumbani,nyumba utapendezesha,
utapokuwa jikoni,chakula kuharakisha,
ukifika sebuleni,karibisho kwa bashasha,
wewe ua la nyumbani,karibu nyumbani kwangu
ua nitaweka wapi,sitaliweka juani,
ua sio kama pipi,zinazouzwa dukani,
ua hilo kwa kifupi si kuweka barazani,
ua ninaloongea,hakika ni wewe Asha.
wimbo gani nikwimbie,yote yamejieleza,
lugha gani nikwambie,upate jipeleleza,
shairi nikutungie lipate kukuliwaza,
vyote unavielewa,jibulo litanipoza
sasa chukua kalamu,jaribu andika kitu,
hata kama kwa awamu,si sawa kuacha katu,
kwa wako utaalamu,utaupenya msitu,
mapenzi sawa msitu,kamanda utaupenya
kama sio kwa shairi,tumia japo kauli,
moyoni itoe siri,iweke kwangu mahali,
jibu nishalikariri,nitoe kwenye muhali
nipe japo taabasamu,liwe ndio jibu lako
mashairi yapo mengi siwezi kuyamaliza
sifa zako zipo nyingi,ngapi nitakueleza,
na vikwazo vipo vingi,najua hutoteleza
gari langu liko wazi na abiiria ni wewe.
sasa ninatua hapa,kuandika kwangu jadi,
kama ni nguvu za papa,karata lasti kadi,
naishia hapahapa,kwako naipiga hodi
hodi nilishaipiga nasubiri kuingia.
SAFARI
safari niliyoanza,Mola ndiye anajua,
nilifikiria kwanza,jibu sikulipatia,
maisha mapya kuanza,yakupasa fikiria,
Maisha kuwa na mwenza,Mola naomba jalia.
siku nyingi niliwaza,atakuwa jinsi gani,
asiwe wa kujikweza,na kuleta tafrani,
awe kujinyenyekeza,siku zote kwa Manani.
Maisha kuwa na mwenza,Mola naomba jalia.
wa ubani kumpata,iligharimu miaka,
sana nilifurukuta,kila mkoa nasaka,
hivi sasa nimepata,moyoni nimemuweka,
Maisha kuwa na mwenza,Mola naomba jalia.
siku tulipoonana,tulikuwa safarini,
sura yake kuiona,nilifurahi moyoni,
ngozi mawaa haina,mfano ya utotoni,
Maisha kuwa na mwenza,Mola naomba jalia.
yeye hana majivuno,kwa kweli ni msikivu,
ukutazama kiuno,na rangi yake angavu
kwa kawaida maono,ni kama mtepetevu
Maisha kuwa na mwenza,Mola naomba jalia.
huyu niliyempata,kwa kweli sifa anazo,
kama ni kwenye karata,kwa kweli garasha sizo,
mizungu nitaikata,rahisi kama pulizo
Maisha kuwa na mwenza,Mola naomba jalia.
jina lake silitaji,naogopa wafitini,
hilo ni sawa mtaji,ninalitunza sirini,
kama ni utafutaji,sikuacha asilani
Maisha kuwa na mwenza,Mola naomba jalia.
nilifikiria kwanza,jibu sikulipatia,
maisha mapya kuanza,yakupasa fikiria,
Maisha kuwa na mwenza,Mola naomba jalia.
siku nyingi niliwaza,atakuwa jinsi gani,
asiwe wa kujikweza,na kuleta tafrani,
awe kujinyenyekeza,siku zote kwa Manani.
Maisha kuwa na mwenza,Mola naomba jalia.
wa ubani kumpata,iligharimu miaka,
sana nilifurukuta,kila mkoa nasaka,
hivi sasa nimepata,moyoni nimemuweka,
Maisha kuwa na mwenza,Mola naomba jalia.
siku tulipoonana,tulikuwa safarini,
sura yake kuiona,nilifurahi moyoni,
ngozi mawaa haina,mfano ya utotoni,
Maisha kuwa na mwenza,Mola naomba jalia.
yeye hana majivuno,kwa kweli ni msikivu,
ukutazama kiuno,na rangi yake angavu
kwa kawaida maono,ni kama mtepetevu
Maisha kuwa na mwenza,Mola naomba jalia.
huyu niliyempata,kwa kweli sifa anazo,
kama ni kwenye karata,kwa kweli garasha sizo,
mizungu nitaikata,rahisi kama pulizo
Maisha kuwa na mwenza,Mola naomba jalia.
jina lake silitaji,naogopa wafitini,
hilo ni sawa mtaji,ninalitunza sirini,
kama ni utafutaji,sikuacha asilani
Maisha kuwa na mwenza,Mola naomba jalia.
PENZI
umenipasha kwa wimbo,kwamba penzi walifuta,
kisa eti vijimambo,vingi ulivyovipata,
umenaswa na ulimbo,hunitaki katakata,
Huyo uliyemuona,ungeuliza ni nani.
ulitoka kwa vikumbo,mlango ulipopita,
na tena kwa majigambo,mabegi uliyavuta,
acha kufata mkumbo,mabaya yatakukuta,
Huyo uliyemuona,ungeuliza ni nani.
kwa ule wako urembo,mimi nilikufuata,
wala sio kwa mapambo,yakanifanya kudata,
kwangu wewe ndio nembo,moyoni imeninata,
Huyo uliyemuona,ungeuliza ni nani.
sitasema kwa mafumbo,penzi lako kulipata,
moyoni unalo jambo,hakika lafurukuta,
usiseme kwa mafumbo,vipi mimi takupata
Huyo uliyemuona,ungeuliza ni nani.
usiyarefushe mambo,huko kwenu nakufata,
hata kama uko Mombo,mtwara hata Msata,
penzi jamani ni fumbo,kamuulize Tilata,
Huyo uliyemuona,ungeuliza ni nani.
halitazami maumbo,penzi likikufuata,
mashaibu kwa vifimbo,maajuza watafuta,
halitizami muambo,popote litajikita
Huyo uliyemuona,ungeuliza ni nani.
kisa eti vijimambo,vingi ulivyovipata,
umenaswa na ulimbo,hunitaki katakata,
Huyo uliyemuona,ungeuliza ni nani.
ulitoka kwa vikumbo,mlango ulipopita,
na tena kwa majigambo,mabegi uliyavuta,
acha kufata mkumbo,mabaya yatakukuta,
Huyo uliyemuona,ungeuliza ni nani.
kwa ule wako urembo,mimi nilikufuata,
wala sio kwa mapambo,yakanifanya kudata,
kwangu wewe ndio nembo,moyoni imeninata,
Huyo uliyemuona,ungeuliza ni nani.
sitasema kwa mafumbo,penzi lako kulipata,
moyoni unalo jambo,hakika lafurukuta,
usiseme kwa mafumbo,vipi mimi takupata
Huyo uliyemuona,ungeuliza ni nani.
usiyarefushe mambo,huko kwenu nakufata,
hata kama uko Mombo,mtwara hata Msata,
penzi jamani ni fumbo,kamuulize Tilata,
Huyo uliyemuona,ungeuliza ni nani.
halitazami maumbo,penzi likikufuata,
mashaibu kwa vifimbo,maajuza watafuta,
halitizami muambo,popote litajikita
Huyo uliyemuona,ungeuliza ni nani.
HIYO SIO MALI YAKO
imenibidi kutunga,kueleza kero hii,
mdomo sitaufunga,naeleza wasanii,
mtasema ninachonga,masimango sisikii,
Hiyo sio mali yako,katu usiichukue.
waingia ofisini,kwa adabu na heshima,
unajitupa kitini,kwa uso wenye huruma,
jicho lako kabatini,kitu umeshakifuma,
Hiyo sio mali yako,katu usiichukue.
ukikutacho mezani,kina makusudi yake,
sikukiweka uani,kinalo jukumu lake,
wakitia mfukoni,nabaki na sekeseke,
Hiyo sio mali yako,katu usiichukue.
ukiisha ichukua,nabaki nawayawaya,
naanza kuangalia,yaweje jamani haya,
hasara niloingia,imeshanitia haya,
Hiyo sio mali yako,katu usiichukue
.
naongea kwa uchungu,mwili unatetemeka,
katu sitaki majungu,ukweli nitauweka,
ukija ofisi yangu,kwanza staarabika,
Hiyo sio mali yako,katu usiichukue.
magazeti na vitabu,vyote wajichukulia,
imeisha kuwa tabu,majonzi unanitia,
ungeeleza sababu,vyote ningekupatia
Hiyo sio mali yako,katu usiichukue
.
hatuwezi piga yowe,kukuita wewe mwizi
unajijua mwenyewe,ziache tabia hizi,
utalili mkwewe,punde tutakumaizi
Hiyo sio mali yako,katu usiichukue.
mdomo sitaufunga,naeleza wasanii,
mtasema ninachonga,masimango sisikii,
Hiyo sio mali yako,katu usiichukue.
waingia ofisini,kwa adabu na heshima,
unajitupa kitini,kwa uso wenye huruma,
jicho lako kabatini,kitu umeshakifuma,
Hiyo sio mali yako,katu usiichukue.
ukikutacho mezani,kina makusudi yake,
sikukiweka uani,kinalo jukumu lake,
wakitia mfukoni,nabaki na sekeseke,
Hiyo sio mali yako,katu usiichukue.
ukiisha ichukua,nabaki nawayawaya,
naanza kuangalia,yaweje jamani haya,
hasara niloingia,imeshanitia haya,
Hiyo sio mali yako,katu usiichukue
.
naongea kwa uchungu,mwili unatetemeka,
katu sitaki majungu,ukweli nitauweka,
ukija ofisi yangu,kwanza staarabika,
Hiyo sio mali yako,katu usiichukue.
magazeti na vitabu,vyote wajichukulia,
imeisha kuwa tabu,majonzi unanitia,
ungeeleza sababu,vyote ningekupatia
Hiyo sio mali yako,katu usiichukue
.
hatuwezi piga yowe,kukuita wewe mwizi
unajijua mwenyewe,ziache tabia hizi,
utalili mkwewe,punde tutakumaizi
Hiyo sio mali yako,katu usiichukue.
HONGERA WAHITIMU
naanza kuwasalimu,ninyi mnaohitimu,
sasa nashika kalamu,kuwapa yale muhimu,
kujali muda muhimu,sote tunaohitimu,
Ingawa mnahitimu,kuwa nanyi twatamani.
mtawaacha walimu,pindi mkijaza fomu,
yawapasa mfahamu,maisha huko magumu,
Mola ndiye ufahamu,hilo budi mfahamu,
Ingawa mnahitimu,kuwa nanyi twatamani.
mmekuwa kama timu,kushinda wote ugumu,
vipindi zamu kwa zamu,waliwafunza walimu,
ili mpate fahamu,mlipokea kwa hamu,
Ingawa mnahitimu,kuwa nanyi twatamani.
Mola mnamfahamu,wa baba yetu Adamu,
Mungu mkamuheshimu,kimafunzo mmedumu,
nanyi ni wana adamu,kutii dumu dawamu,
Ingawa mnahitimu,kuwa nanyi twatamani.
hakika mmefahamu,elimu ni ya muhimu,
mtakuwa watalamu,umma kuupa fahamu,
yale mlopata humu,jalini ubinadamu
Ingawa mnahitimu,kuwa nanyi twatamani.
sasa nashika kalamu,kuwapa yale muhimu,
kujali muda muhimu,sote tunaohitimu,
Ingawa mnahitimu,kuwa nanyi twatamani.
mtawaacha walimu,pindi mkijaza fomu,
yawapasa mfahamu,maisha huko magumu,
Mola ndiye ufahamu,hilo budi mfahamu,
Ingawa mnahitimu,kuwa nanyi twatamani.
mmekuwa kama timu,kushinda wote ugumu,
vipindi zamu kwa zamu,waliwafunza walimu,
ili mpate fahamu,mlipokea kwa hamu,
Ingawa mnahitimu,kuwa nanyi twatamani.
Mola mnamfahamu,wa baba yetu Adamu,
Mungu mkamuheshimu,kimafunzo mmedumu,
nanyi ni wana adamu,kutii dumu dawamu,
Ingawa mnahitimu,kuwa nanyi twatamani.
hakika mmefahamu,elimu ni ya muhimu,
mtakuwa watalamu,umma kuupa fahamu,
yale mlopata humu,jalini ubinadamu
Ingawa mnahitimu,kuwa nanyi twatamani.
PESA WAPELEKA WAPI?
wengi watanishangaa,kuuliza swali hili,
wengine watazubaa,kuniita mswahili,
maswali yatazagaa,eti nifunge bakuli,
pesa wapeleka wapi,mbona mambo hayaendi?
nguo zako rapurapu,kwako viatu ni ndala,
wabugia taputapu,kwako imekuwa sala,
imebadilika shepu,kama nguruwe wa Ngwala,
pesa wapeleka wapi,mbona mambo hayaendi?
mkeo alalamika,hali nyumbani ni ngumu,
vitumbua anapika,kuupunguza ugumu,
kwenye pombe watukuka,nyumbani pesa ni ngumu,
pesa wapeleka wapi,mbona mambo hayaendi?
mumeo alalamika,kwamba haueleweki,
wapi unazipeleka,au chini ya kasiki,
wewe unajibweteka,mbona hauambilki,
pesa wapeleka wapi,mbona mambo hayaendi?
wazazi wajiuliza,hata ndugu zako pia,
umebaki kuwaliza,macho wanayatumbua,
sana umewachukiza,wapweke wamebakia,
pesa wapeleka wapi,mbona mambo hayaendi?
wengine watazubaa,kuniita mswahili,
maswali yatazagaa,eti nifunge bakuli,
pesa wapeleka wapi,mbona mambo hayaendi?
nguo zako rapurapu,kwako viatu ni ndala,
wabugia taputapu,kwako imekuwa sala,
imebadilika shepu,kama nguruwe wa Ngwala,
pesa wapeleka wapi,mbona mambo hayaendi?
mkeo alalamika,hali nyumbani ni ngumu,
vitumbua anapika,kuupunguza ugumu,
kwenye pombe watukuka,nyumbani pesa ni ngumu,
pesa wapeleka wapi,mbona mambo hayaendi?
mumeo alalamika,kwamba haueleweki,
wapi unazipeleka,au chini ya kasiki,
wewe unajibweteka,mbona hauambilki,
pesa wapeleka wapi,mbona mambo hayaendi?
wazazi wajiuliza,hata ndugu zako pia,
umebaki kuwaliza,macho wanayatumbua,
sana umewachukiza,wapweke wamebakia,
pesa wapeleka wapi,mbona mambo hayaendi?
ENDESHA GARI VIZURI
udereva kazi ngumu,sana ukifikiria,
kuendesha ni vigumu,sukani kushikilia,
umakini ni muhimu,ajali sije tokea,
Endesha gari vizuri,ajali kuziepuka.
gari unaliendesha,kwa raha mustarehe,
njiani unatushusha,hata kwenye masherehe,
safari kweli yachosha,pamoja ni starehe,
Endesha gari vizuri,ajali kuziepuka.
gari hili tuthamini,kila mtu alipenda,
unapofika kitini,ni wasaa kulipenda,
mafuta simwage chini,ni sawa pesa kuponda,
Endesha gari vizuri,ajali kuziepuka.
kiti ni cha kukalia,sio kusimama juu,
matope watupakia,hatuyapendi makuu,
sasa hivi umekua,wewe sio mjukuu,
Endesha gari vizuri,ajali kuziepuka.
gia nikanyage vipi,mafuta yamezagaa,
miguu niweke wapi,nimebaki nashangaa,
hili gari ni kwa vipi,mafuta yatapakaa,
Endesha gari vizuri,ajali kuziepuka.
kuendesha ni vigumu,sukani kushikilia,
umakini ni muhimu,ajali sije tokea,
Endesha gari vizuri,ajali kuziepuka.
gari unaliendesha,kwa raha mustarehe,
njiani unatushusha,hata kwenye masherehe,
safari kweli yachosha,pamoja ni starehe,
Endesha gari vizuri,ajali kuziepuka.
gari hili tuthamini,kila mtu alipenda,
unapofika kitini,ni wasaa kulipenda,
mafuta simwage chini,ni sawa pesa kuponda,
Endesha gari vizuri,ajali kuziepuka.
kiti ni cha kukalia,sio kusimama juu,
matope watupakia,hatuyapendi makuu,
sasa hivi umekua,wewe sio mjukuu,
Endesha gari vizuri,ajali kuziepuka.
gia nikanyage vipi,mafuta yamezagaa,
miguu niweke wapi,nimebaki nashangaa,
hili gari ni kwa vipi,mafuta yatapakaa,
Endesha gari vizuri,ajali kuziepuka.
Monday, September 19, 2011
WAZAZI
wazazi tulionao,ni mola katujalia,
hata kama haunao,Muumba kawachukua,
aliwapa na uzao,watoto kawapatia.
wazazi tulionao,halahala tuwatunze.
mola kawapa ukoo,unaoweza kukua,
si kama ule wa koo,watoto kutowalea,
watoto sio popoo,yapasa kuangalia,
wazazi tulionao,halahala tuwatunze.
tusikabane makoo,pesa ili watumia,
sana twalizua soo,usoweza fikiria,
wao si kidali poo,kuweza kuwachezea,
wazazi tulionao,halahala tuwatunze.
hebu tazama kioo,ndiko walikotokea,
hauhitaji apio,ujana walipitia,
wewe sawa na minyoo,wazazi kuwachukia,
wazazi tulionao,halahala tuwatunze.
wao wakisema ndio,baraka utapokea,
baraka watoa wao,mambo yatunyookea,
wao sawa na kinoo,njia kutusafishia,
wazazi tulionao,halahala tuwatunze.
hata kama haunao,Muumba kawachukua,
aliwapa na uzao,watoto kawapatia.
wazazi tulionao,halahala tuwatunze.
mola kawapa ukoo,unaoweza kukua,
si kama ule wa koo,watoto kutowalea,
watoto sio popoo,yapasa kuangalia,
wazazi tulionao,halahala tuwatunze.
tusikabane makoo,pesa ili watumia,
sana twalizua soo,usoweza fikiria,
wao si kidali poo,kuweza kuwachezea,
wazazi tulionao,halahala tuwatunze.
hebu tazama kioo,ndiko walikotokea,
hauhitaji apio,ujana walipitia,
wewe sawa na minyoo,wazazi kuwachukia,
wazazi tulionao,halahala tuwatunze.
wao wakisema ndio,baraka utapokea,
baraka watoa wao,mambo yatunyookea,
wao sawa na kinoo,njia kutusafishia,
wazazi tulionao,halahala tuwatunze.
TURUDI KWETU
watu wetu watu wetu,sasa na turudi kwetu,
huko sasa sio kwetu,turudi na vitu vyetu,
sipapendi huko katu,twapoteza mila zetu,
sasa na turudi kwetu,tujivunie vya kwetu.
nimeona vitu vingi,sisemi uongo katu,
pia nimeona watu,akili zao ni fyatu,
hila mfano wa chatu,au sawa mbwa mwitu,
Jamani tutafakari,tupate ndoa imara.
utamaduni si wetu,tujivunie vya kwetu,
vimini si jadi yetu,suruali sio zetu,
pedo sitavaa katu,kwani mimi si kifutu,
Jamani tutafakari,tupate ndoa imara.
sasa sisi tuwe watu,tuenzi taifa letu,
kuiga mila za watu,twaua vizazi vyetu,
mila si sawa viatu,kuvaa vya kila mtu
Jamani tutafakari,tupate ndoa imara.
huko sasa sio kwetu,turudi na vitu vyetu,
sipapendi huko katu,twapoteza mila zetu,
sasa na turudi kwetu,tujivunie vya kwetu.
nimeona vitu vingi,sisemi uongo katu,
pia nimeona watu,akili zao ni fyatu,
hila mfano wa chatu,au sawa mbwa mwitu,
Jamani tutafakari,tupate ndoa imara.
utamaduni si wetu,tujivunie vya kwetu,
vimini si jadi yetu,suruali sio zetu,
pedo sitavaa katu,kwani mimi si kifutu,
Jamani tutafakari,tupate ndoa imara.
sasa sisi tuwe watu,tuenzi taifa letu,
kuiga mila za watu,twaua vizazi vyetu,
mila si sawa viatu,kuvaa vya kila mtu
Jamani tutafakari,tupate ndoa imara.
TUTAFAKARI
ndoa ni kitu kizuri,sana ukitafakari,
nyingi kama utiriri,nyingi sana zina heri,
hebu jaribu fikiri,uone wake uzuri,
Jamani tutafakari,tupate ndoa imara.
mambo mengi yanajiri,hebu tuache kiburi,
ndoa si sawa futari,inataka umahiri,
ndoa sio kukariri,ndani ya madaftari,
Jamani tutafakari,tupate ndoa imara.
ndoa hakika safari,inataka wenye heri,
ukijitia kafiri,utaiona saburi,
yapasa uwe mahiri,kushinda hiyo safari
Jamani tutafakari,tupate ndoa imara.
ndoa ni kitu kizuri,hupaswi kuwa na mori,
usiwe nayo jeuri,kama vile paka pori,
ukijitia mpori,tengano lawasubiri,
Jamani tutafakari,tupate ndoa imara.
nyingi kama utiriri,nyingi sana zina heri,
hebu jaribu fikiri,uone wake uzuri,
Jamani tutafakari,tupate ndoa imara.
mambo mengi yanajiri,hebu tuache kiburi,
ndoa si sawa futari,inataka umahiri,
ndoa sio kukariri,ndani ya madaftari,
Jamani tutafakari,tupate ndoa imara.
ndoa hakika safari,inataka wenye heri,
ukijitia kafiri,utaiona saburi,
yapasa uwe mahiri,kushinda hiyo safari
Jamani tutafakari,tupate ndoa imara.
ndoa ni kitu kizuri,hupaswi kuwa na mori,
usiwe nayo jeuri,kama vile paka pori,
ukijitia mpori,tengano lawasubiri,
Jamani tutafakari,tupate ndoa imara.
MWALIMU
kila mtu ni mwalimu,tofauti taaluma,
wapo wa mambo muhimu,na wengine maamuma,
wapi tapata rasimu,sipendi jiumauma,
kila mtu ni mwalimu,wengi si kitaaluma,
akufundishaye jambo,huyo kwako ni mwalimu,
hata kama kwa vikumbo,sheria utasalimu,
wataka kujua mambo,hutoogopa hukumu,
kila mtu ni mwalimu,wengi si kitaaluma,
baba aliyekuzaa,huyo ni mwalimu wako,
mama aliyekulea,naye ni mwalimu wako,
jirani penye mtaa,ajua tabia zako,
kila mtu ni mwalimu,wengi si kitaaluma,
yule babako mzazi,yeye ni mwalimu wako,
akifanya ubazazi,hiyo ni elimu yako,
kama yeye mchochezi,huo ni urithi wako,
kila mtu ni mwalimu,wengi si kitaaluma,
mama mpika majungu,hiyo ni elimu yako,
wamsuta kwa uchungu,kwake yeye ni karamu,
enda chini ya uvungu,ni wapi mwana adamu,
kila mtu ni mwalimu,wengi si kitaaluma,
baba kutwa amenuna,anawapa somo gani,
hakuna raha hakuna,watu wote ni huzuni,
watoto wakikuona,hujificha uvunguni,
kila mtu ni mwalimu,wengi si kitaaluma,
wapo wa mambo muhimu,na wengine maamuma,
wapi tapata rasimu,sipendi jiumauma,
kila mtu ni mwalimu,wengi si kitaaluma,
akufundishaye jambo,huyo kwako ni mwalimu,
hata kama kwa vikumbo,sheria utasalimu,
wataka kujua mambo,hutoogopa hukumu,
kila mtu ni mwalimu,wengi si kitaaluma,
baba aliyekuzaa,huyo ni mwalimu wako,
mama aliyekulea,naye ni mwalimu wako,
jirani penye mtaa,ajua tabia zako,
kila mtu ni mwalimu,wengi si kitaaluma,
yule babako mzazi,yeye ni mwalimu wako,
akifanya ubazazi,hiyo ni elimu yako,
kama yeye mchochezi,huo ni urithi wako,
kila mtu ni mwalimu,wengi si kitaaluma,
mama mpika majungu,hiyo ni elimu yako,
wamsuta kwa uchungu,kwake yeye ni karamu,
enda chini ya uvungu,ni wapi mwana adamu,
kila mtu ni mwalimu,wengi si kitaaluma,
baba kutwa amenuna,anawapa somo gani,
hakuna raha hakuna,watu wote ni huzuni,
watoto wakikuona,hujificha uvunguni,
kila mtu ni mwalimu,wengi si kitaaluma,
NIAMBIE
kuna jambo lakutinga,nakuomba niambie,
lipo jambo ulipanga,bora nifafanulie,
ni mawazo yakusonga,si' tukufafanulie,
kaza moyo niambie,ni lipi linakutinga.
twaishi sote chumbani,mimi nikiwa mkeo,
usilete tafrani,ninalueleza leo,
sura yako taabani,mikunjo bila mkao,
juzi uliniambia,wataka mke wa pili,
mimi niliridhia,tamaa zako za mwili,
macho leo nikazia,tena ni mwezi kamili,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
uchumba tulipoanza,wala hukuleta manza,
ni wewe ulinianza,kunitoa kwetu Mwanza,
imani imeniponza,tangu uchumba kuaanza,
Kaza moyo niambie,ni lipi linakusibu
kutwa kucha umenuna,nyumbani hapakaliki,
wiki tatu nimeona,jikoni hapapikiki,
siwezi hata jikuna,sebule haikalilki,
. Kaza moyo niambie,ni lipi linakusibu
kwetu jiko haliwaki,wewe unakula wapi,
uyafanyayo si haki,hata kama ni kwa 'popi;,
wewe wala mishikaki,mimi ni maji na pipi,
Kaza moyo niambie,ni lipi linakusibundoa kitu cha hiyari,sio kulazimishana,
kaa vizuri fikiri,tusije ngeo toana,
moyoni nilitabiri,siku tutafarakana,
Kaza moyo niambie,ni lipi linakusibu
umeshindwa kunambia,mimi nasema nakwenda,
sipendi kuambulia,kwa wenzio kuniponda,
Mungu atanijalia,raha nami nitaponda
Kaza moyo niambie,ni lipi linakusibu.
lipo jambo ulipanga,bora nifafanulie,
ni mawazo yakusonga,si' tukufafanulie,
kaza moyo niambie,ni lipi linakutinga.
twaishi sote chumbani,mimi nikiwa mkeo,
usilete tafrani,ninalueleza leo,
sura yako taabani,mikunjo bila mkao,
juzi uliniambia,wataka mke wa pili,
mimi niliridhia,tamaa zako za mwili,
macho leo nikazia,tena ni mwezi kamili,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
uchumba tulipoanza,wala hukuleta manza,
ni wewe ulinianza,kunitoa kwetu Mwanza,
imani imeniponza,tangu uchumba kuaanza,
Kaza moyo niambie,ni lipi linakusibu
kutwa kucha umenuna,nyumbani hapakaliki,
wiki tatu nimeona,jikoni hapapikiki,
siwezi hata jikuna,sebule haikalilki,
. Kaza moyo niambie,ni lipi linakusibu
kwetu jiko haliwaki,wewe unakula wapi,
uyafanyayo si haki,hata kama ni kwa 'popi;,
wewe wala mishikaki,mimi ni maji na pipi,
Kaza moyo niambie,ni lipi linakusibundoa kitu cha hiyari,sio kulazimishana,
kaa vizuri fikiri,tusije ngeo toana,
moyoni nilitabiri,siku tutafarakana,
Kaza moyo niambie,ni lipi linakusibu
umeshindwa kunambia,mimi nasema nakwenda,
sipendi kuambulia,kwa wenzio kuniponda,
Mungu atanijalia,raha nami nitaponda
Kaza moyo niambie,ni lipi linakusibu.
ULIDHANI UNAJUA
hakika wajidanganya,ukidhani ni mwezio,
urafiki mlifanya,tena kwa mafanikio,
akili hukuikanya,tena kwa mfatilio,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
shule mlisoma wote,na tena darasa moja,
mliongozana kote,tena kwa ule umoja,
mpira kucheza nyote,mlikuwa halimoja,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
mtaa wenu mmoja,tena kuitana ndugu,
sisi mnazimmoja,na yeye kwao ni Pugu,
jambo tulilolingoja,sasa imekuwa pwagu,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
wakumbuke marafiki,mlipokuwa watoto,
hamkuwa wanafiki,mambo kufanya mkato,
hata nawe wasadiki,mambo yote motomoto,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
leo hii mmekua,mnapigiana simu,
ahadi mwajipangia,kila mtu ana hamu,
barua wamwandikia,tena huna urasimu,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
mkomba yuko Kahama,na wewe una hakika,
atakwambia kahama,anazo nyingi pilika,
kumbe huko amekwama,kimaisha kapigika,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
unampigia Ali,rafiki yako kipenzi,
ukamlilie hali,unazikumbuka enzi,
Ali sasa hakujali,wamghasi kama nzi,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
urafiki mlifanya,tena kwa mafanikio,
akili hukuikanya,tena kwa mfatilio,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
shule mlisoma wote,na tena darasa moja,
mliongozana kote,tena kwa ule umoja,
mpira kucheza nyote,mlikuwa halimoja,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
mtaa wenu mmoja,tena kuitana ndugu,
sisi mnazimmoja,na yeye kwao ni Pugu,
jambo tulilolingoja,sasa imekuwa pwagu,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
wakumbuke marafiki,mlipokuwa watoto,
hamkuwa wanafiki,mambo kufanya mkato,
hata nawe wasadiki,mambo yote motomoto,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
leo hii mmekua,mnapigiana simu,
ahadi mwajipangia,kila mtu ana hamu,
barua wamwandikia,tena huna urasimu,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
mkomba yuko Kahama,na wewe una hakika,
atakwambia kahama,anazo nyingi pilika,
kumbe huko amekwama,kimaisha kapigika,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
unampigia Ali,rafiki yako kipenzi,
ukamlilie hali,unazikumbuka enzi,
Ali sasa hakujali,wamghasi kama nzi,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
Sunday, September 18, 2011
ULIDHANI UNAJUA
hakika wajidanganya,ukidhani ni mwenzako,
urafiki mlifanya tena kwa mafanikio,
akili hukuikanya,tena kwa mfatilio,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
shule mlisoma wote,na tena darasa moja,
mliongozana kote,tena kwa ule umoja,
mpira kucheza wote,mlikuwa halimoja,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
mtaa wenu mmoja,tena kuitana ndugu,
sisi mnazi mmoja,na wao kwao ni Pugu,
jambo tulilolingoja sasa imekuwa pwagu
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
wakumbuke marafiki,mlipokuwa watoto
urafiki mlifanya tena kwa mafanikio,
akili hukuikanya,tena kwa mfatilio,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
shule mlisoma wote,na tena darasa moja,
mliongozana kote,tena kwa ule umoja,
mpira kucheza wote,mlikuwa halimoja,
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
mtaa wenu mmoja,tena kuitana ndugu,
sisi mnazi mmoja,na wao kwao ni Pugu,
jambo tulilolingoja sasa imekuwa pwagu
Ulidhani unajua,kumbe unajidanganya.
wakumbuke marafiki,mlipokuwa watoto
CHAMA
chama hiki chama chetu,sote tunalitambua,
chama kinajali utu,sote tunakiimbia,
sio chama cha upatu,pesa kikatuibia,
chama kikishakuchoka,hakika utagundua.
mialiko ya kichama,katu hutoisikia,
ulizoea 'minyama',hata supu ya mkia,
kujirusha na 'mimama',hata na vichangudoa,
chama kikishakuchoka,hakika utagundua.
shangingi hutolipanda,miguu yako ni gari,
mwanga ulioupenda,wako sasa kibatari,
hivi sasa wakuponda,kama ya jana futari,
chama kikishakuchoka,hakika utagundua.
chama kinajali utu,sote tunakiimbia,
sio chama cha upatu,pesa kikatuibia,
chama kikishakuchoka,hakika utagundua.
mialiko ya kichama,katu hutoisikia,
ulizoea 'minyama',hata supu ya mkia,
kujirusha na 'mimama',hata na vichangudoa,
chama kikishakuchoka,hakika utagundua.
shangingi hutolipanda,miguu yako ni gari,
mwanga ulioupenda,wako sasa kibatari,
hivi sasa wakuponda,kama ya jana futari,
chama kikishakuchoka,hakika utagundua.
KWA NINI?
mimi nawaza kwa nini,inatokea kwa nini,
mkono kuwa shavuni,nikiwapo mawazoni,
mbona siweki begani,au kuweka shingoni,
Nini kinasababisha,mkono kuwa shavuni?
hata kwenye mitihani,wewe jaribu chunguza,
akili zipo kichwani,sana muda utawaza,
mkono upo shavuni,kichwani kupeleleza,
Nini kinasababisha,mkono kuwa shavuni?
habari ya kushtusha,mikono kuwa kichwani,
kwa nini hukuishusha,kuipeleka shavuni,
sasa nini chakuchosha,jijadili akilini,
Nini kinasababisha,mkono kuwa shavuni?
jambo linalokutisha,waiweka na kutoa,
lile la kusikitisha,shavuni wajiwekea,
mawazo yakikutosha,waenda kujilalia
Nini kinasababisha,mkono kuwa shavuni?
mkono kuwa shavuni,nikiwapo mawazoni,
mbona siweki begani,au kuweka shingoni,
Nini kinasababisha,mkono kuwa shavuni?
hata kwenye mitihani,wewe jaribu chunguza,
akili zipo kichwani,sana muda utawaza,
mkono upo shavuni,kichwani kupeleleza,
Nini kinasababisha,mkono kuwa shavuni?
habari ya kushtusha,mikono kuwa kichwani,
kwa nini hukuishusha,kuipeleka shavuni,
sasa nini chakuchosha,jijadili akilini,
Nini kinasababisha,mkono kuwa shavuni?
jambo linalokutisha,waiweka na kutoa,
lile la kusikitisha,shavuni wajiwekea,
mawazo yakikutosha,waenda kujilalia
Nini kinasababisha,mkono kuwa shavuni?
KUKAA KIMYA
Tafsiri nimejua,mtu jibu kutotoa,
sana anafikiria,vipi atakupatia,
pengine anadhania,ni vigumu kuongea,
Kila akaaye kimya,jibu lake ni mwanana.
Si lazima akwambie,ndipo ulipate jibu,
wala umsogelee,awe japo kwa karibu,
au sana muongee,ajifunue hijabu,
Kila akaaye kimya,jibu lake ni mwanana.
sana anafikiria,vipi atakupatia,
pengine anadhania,ni vigumu kuongea,
Kila akaaye kimya,jibu lake ni mwanana.
Si lazima akwambie,ndipo ulipate jibu,
wala umsogelee,awe japo kwa karibu,
au sana muongee,ajifunue hijabu,
Kila akaaye kimya,jibu lake ni mwanana.
Friday, September 16, 2011
TUJENGE NYUMBA ZETU
upangaji kazi ngumu,hakika nimeamini,
nimeona umuhimu,niandike gazetini,
utakayosoma humu,nimeona kwa jirani,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
mijini tunamoishi,kuna mambo ya ajabu,
haihitaji ubishi,itakuja kupa tabu,
huwezi kamata moshi ,bure utajisulubu,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
kweli kodi tunalipa tena gharama ya juu,
sio kwamba twajitapa,hatuyapendi makuu,
umetukumba 'ukapa',neno hilo nanukuu,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
umeme bei wapanga,bila kuonyesha bili,
kosa langu ni kupanga,huu ni mwaka wa pili,
usidhani mi mchanga,nilipe elfu mbili,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
nikichelewa kidogo,geti tayari wafunga,
mimi sina nyumba ndogo,mbili siwezi kupanga,
sa' mbili muda mdogo,kazi zinaponitinga,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
siku moja nakumbuka,wiki moja ulinuna,
nini kilichokufika,hata salamu hakuna,
kumbe siku ilifika,mfukoni pesa huna,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
ukweli tabu twapata,sisi tusio na nyumba,
shida zianpotupata,wao macho wanafumba,
hawaujui ukata,wataka kodi ya nyumba,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
kulipa kodi ni haki,hiyo wote tunajua,
chumba umenipa hiki,na jiko la kupikia,
usinijengee chuki,kodi nitakupatia,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
nyumba yangu nikijenga,sana nitafurahia,
vyumba nitavyovipanga,wengi mtatamania,
nitakuacha kupanga,maisha kufurahia,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
tamati sasa nafika,pia namuomba mungu,
na wakati ukifika,niijenge nyumba yangu,
tabu zilizonifika,zinanitia uchungu,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
nimeona umuhimu,niandike gazetini,
utakayosoma humu,nimeona kwa jirani,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
mijini tunamoishi,kuna mambo ya ajabu,
haihitaji ubishi,itakuja kupa tabu,
huwezi kamata moshi ,bure utajisulubu,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
kweli kodi tunalipa tena gharama ya juu,
sio kwamba twajitapa,hatuyapendi makuu,
umetukumba 'ukapa',neno hilo nanukuu,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
umeme bei wapanga,bila kuonyesha bili,
kosa langu ni kupanga,huu ni mwaka wa pili,
usidhani mi mchanga,nilipe elfu mbili,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
nikichelewa kidogo,geti tayari wafunga,
mimi sina nyumba ndogo,mbili siwezi kupanga,
sa' mbili muda mdogo,kazi zinaponitinga,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
siku moja nakumbuka,wiki moja ulinuna,
nini kilichokufika,hata salamu hakuna,
kumbe siku ilifika,mfukoni pesa huna,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
ukweli tabu twapata,sisi tusio na nyumba,
shida zianpotupata,wao macho wanafumba,
hawaujui ukata,wataka kodi ya nyumba,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
kulipa kodi ni haki,hiyo wote tunajua,
chumba umenipa hiki,na jiko la kupikia,
usinijengee chuki,kodi nitakupatia,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
nyumba yangu nikijenga,sana nitafurahia,
vyumba nitavyovipanga,wengi mtatamania,
nitakuacha kupanga,maisha kufurahia,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
tamati sasa nafika,pia namuomba mungu,
na wakati ukifika,niijenge nyumba yangu,
tabu zilizonifika,zinanitia uchungu,
Ukijenga nyumba yako,hakika utatulia.
SINA UHAKIKA
mimi bado ni mdogo,swali siwezi kujibu,
swali halina udogo,kupata lake jawabu,
huyu babetu mdogo,wote kwetu ni ajabu,
bado hakika sinayo,huyu ndiye baba yetu.
nimeona baba wengi,tena na zao busara,
wenye watoto kwa wingi,hata kama ni fukara,
upendo kwao ni mwingi,uliojaa tijara,
bado hakika sinayo,huyu ndiye baba yetu.
baba ananishangaza,kweli hana shukrani,
kutwa anajitangaza,eti anatuthamini,
kazi yake kujikweza,eti yeye wa thamani,
bado hakika sinayo,huyu ndiye baba yetu.
kama angekuwa wetu,asingekuwa muoga,
kama tatizo ni letu,angesema bila woga,
angetupa haki yetu,watoto sio mizoga,
bado hakika sinayo,huyu ndiye baba yetu.
mama yetu hatunaye,jibu angetupatia,
baba ambaye tunaye,mashaka twamtilia,
hivi kweli ndiye yeye,jirani twaulizia,
bado hakika sinayo,huyu ndiye baba yetu.
swali halina udogo,kupata lake jawabu,
huyu babetu mdogo,wote kwetu ni ajabu,
bado hakika sinayo,huyu ndiye baba yetu.
nimeona baba wengi,tena na zao busara,
wenye watoto kwa wingi,hata kama ni fukara,
upendo kwao ni mwingi,uliojaa tijara,
bado hakika sinayo,huyu ndiye baba yetu.
baba ananishangaza,kweli hana shukrani,
kutwa anajitangaza,eti anatuthamini,
kazi yake kujikweza,eti yeye wa thamani,
bado hakika sinayo,huyu ndiye baba yetu.
kama angekuwa wetu,asingekuwa muoga,
kama tatizo ni letu,angesema bila woga,
angetupa haki yetu,watoto sio mizoga,
bado hakika sinayo,huyu ndiye baba yetu.
mama yetu hatunaye,jibu angetupatia,
baba ambaye tunaye,mashaka twamtilia,
hivi kweli ndiye yeye,jirani twaulizia,
bado hakika sinayo,huyu ndiye baba yetu.
ACHA KUONGOPA
umezidi kuongopa,watu tunakuogopa,
uongo unaotupa,ni shetani amekupa,
kwa Mungu ungejitupa,ni baraka angekupa,
uongo ulionao,wote tunakuogopa.
ulisema kaka yako,ni msaidizi wako,
kumbe halikuwa kwako,bali ni kinywani mwako,
kumfanya mbwa koko,au ya embe makoko,
uongo ulionao,wote tunakuogopa.
ulisemalo kinywani,kumbe hunalo moyoni,
watufanya hayawani,kama kitanda chumbani,
kutoka mkutanoni,waeleza vilabuni,
uongo ulionao,wote tunakuogopa.
janga litapokukumba,tamlilia muumba,
sasa mali unatimba,umesahau kuomba,
wafanya hata vilemba,umekuwa sawa mamba,
uongo ulionao,wote tunakuogopa.
uongo unaotupa,ni shetani amekupa,
kwa Mungu ungejitupa,ni baraka angekupa,
uongo ulionao,wote tunakuogopa.
ulisema kaka yako,ni msaidizi wako,
kumbe halikuwa kwako,bali ni kinywani mwako,
kumfanya mbwa koko,au ya embe makoko,
uongo ulionao,wote tunakuogopa.
ulisemalo kinywani,kumbe hunalo moyoni,
watufanya hayawani,kama kitanda chumbani,
kutoka mkutanoni,waeleza vilabuni,
uongo ulionao,wote tunakuogopa.
janga litapokukumba,tamlilia muumba,
sasa mali unatimba,umesahau kuomba,
wafanya hata vilemba,umekuwa sawa mamba,
uongo ulionao,wote tunakuogopa.
Thursday, September 15, 2011
LEA WATOTO VIZURI
Mungu amewabariki,uzao kuwapatia,
kupata wana riziki,ni mola akijalia,
haihitaji mikiki,Mola ndiye anatoa,
Lea watoto vizuri,kuwatesa ni laana.
wengi wanahangaika,kwenda hata kwa waganga,
kwingi wanazunguuka,wafika hata ulanga,
wanazidi kuzuzuka,hata wajifunza wanga,
Lea watoto vizuri,kuwatesa ni laana.
mara nyingi nashangaa,wengi watupa watoto,
huruma inatujaa,haya ni gani mapito,
watoto tunaozaa,ubora zaidi vito,
Lea watoto vizuri,kuwatesa ni laana.
wengineo washangaza,watoto wingi wa timu,
kwa watu wajitangaza,kuzaa kwao si zamu,
nguo zao zaongoza,viraka zamu kwa zamu,
Lea watoto vizuri,kuwatesa ni laana.
kama chakula wapate,kingi cha kutosheleza,
asubuhi kwa mkate,hata kwa wali na pweza,
matunda ukayapate,afya zao utakuza
Lea watoto vizuri,kuwatesa ni laana.
kupata wana riziki,ni mola akijalia,
haihitaji mikiki,Mola ndiye anatoa,
Lea watoto vizuri,kuwatesa ni laana.
wengi wanahangaika,kwenda hata kwa waganga,
kwingi wanazunguuka,wafika hata ulanga,
wanazidi kuzuzuka,hata wajifunza wanga,
Lea watoto vizuri,kuwatesa ni laana.
mara nyingi nashangaa,wengi watupa watoto,
huruma inatujaa,haya ni gani mapito,
watoto tunaozaa,ubora zaidi vito,
Lea watoto vizuri,kuwatesa ni laana.
wengineo washangaza,watoto wingi wa timu,
kwa watu wajitangaza,kuzaa kwao si zamu,
nguo zao zaongoza,viraka zamu kwa zamu,
Lea watoto vizuri,kuwatesa ni laana.
kama chakula wapate,kingi cha kutosheleza,
asubuhi kwa mkate,hata kwa wali na pweza,
matunda ukayapate,afya zao utakuza
Lea watoto vizuri,kuwatesa ni laana.
MTU ANAPOKUUDHI
hakika inachukiza,ukorofi ukianza,
tena inaleta kiza,mtu manza akianza,
na pia inatatiza,vurugu inapoanza,
mtu akikukosea,jitahidi msamehe.
wengi wananishangaza,pindi wanapochukia,
huanza na kutangaza,wanashindwa kutulia,
hasira wanazijaza,busara yatokomea,
mtu akikukosea,jitahidi msamehe.
mtu anapokukosa,ni budi mfikiria,
hekima ukiikosa,hasira itatopea,
huruma utaikosa,mbumbumbu utabakia,
mtu akikukosea,jitahidi msamehe.
mimi sana nashangaa,ugomvi unapoanza,
chanzo ukifikiria,sababu zipate kwanza,
sio mambo kurukia,utakuja kujiponza,
mtu akikukosea,jitahidi msamehe.
ugomvi kitu kibaya,mimi ninakichukia,
tena unatia haya,nikianza simulia,
mambo haya ni mabaya,sipendi yakitokea,
mtu akikukosea,jitahidi msamehe.
kama wewe umekosa,kamuombe samahani,
usimuwekee visa,hasira hutaiwini,
usivifunge vitasa,vya sanduku la amani,
mtu akikukosea,jitahidi msamehe.
kusamehe kazi ngumu,usipo muomba Mungu,
ukipata jambo gumu,kufikiri ni muhimu,
usifanye kichwa ngumu,msamaha walazimu,
mtu akikukosea,jitahidi msamehe.
tena inaleta kiza,mtu manza akianza,
na pia inatatiza,vurugu inapoanza,
mtu akikukosea,jitahidi msamehe.
wengi wananishangaza,pindi wanapochukia,
huanza na kutangaza,wanashindwa kutulia,
hasira wanazijaza,busara yatokomea,
mtu akikukosea,jitahidi msamehe.
mtu anapokukosa,ni budi mfikiria,
hekima ukiikosa,hasira itatopea,
huruma utaikosa,mbumbumbu utabakia,
mtu akikukosea,jitahidi msamehe.
mimi sana nashangaa,ugomvi unapoanza,
chanzo ukifikiria,sababu zipate kwanza,
sio mambo kurukia,utakuja kujiponza,
mtu akikukosea,jitahidi msamehe.
ugomvi kitu kibaya,mimi ninakichukia,
tena unatia haya,nikianza simulia,
mambo haya ni mabaya,sipendi yakitokea,
mtu akikukosea,jitahidi msamehe.
kama wewe umekosa,kamuombe samahani,
usimuwekee visa,hasira hutaiwini,
usivifunge vitasa,vya sanduku la amani,
mtu akikukosea,jitahidi msamehe.
kusamehe kazi ngumu,usipo muomba Mungu,
ukipata jambo gumu,kufikiri ni muhimu,
usifanye kichwa ngumu,msamaha walazimu,
mtu akikukosea,jitahidi msamehe.
TUSIBAGUE WATOTO
mtoto akizaliwa,lazima apewe jina,
kupata ni majaliwa,kulazimisha hapana,
hakika nimeelewa,kwa marefu na mapana,
Tumieni jina langu,na sio mama fulani
mara nyingi nimeona,matumizi ya majina,
mengi yanavyofanana,na tena yanagongana,.
watu wanapoitana,majina yao mwanana,
Tumieni jina langu,na sio mama fulani
mimi ninaye mtoto,jina aitwa aleni,
sijampata kwa ndoto,kanipatia manani,
haikuwa wangu wito,sasa ninaye nyumbani,
Tumieni jina langu,na sio mama fulani
akijalia manani,wazazi zawadi kuu,
jina lako ni jamali,katu sipende makuu,
mtoto wako ni Ali,wewe baba ya Abuu,
Tumieni jina langu,na sio mama fulani
unabagua watoto,kutumia jina moja,
wewe ni mama Kizito,mumeo baba Mhoja,
wajiita mama wini,sisi watupa utata,
Tumieni jina langu,na sio mama fulani
watoto kuwabagua,ni dhambi kubwa kwa Mola,
jina moja wachagua,ndugu yangu Halahala,
baba John nakwambia,kamwambie na Hamala,
Tumieni jina langu,na sio mama fulani
kupata ni majaliwa,kulazimisha hapana,
hakika nimeelewa,kwa marefu na mapana,
Tumieni jina langu,na sio mama fulani
mara nyingi nimeona,matumizi ya majina,
mengi yanavyofanana,na tena yanagongana,.
watu wanapoitana,majina yao mwanana,
Tumieni jina langu,na sio mama fulani
mimi ninaye mtoto,jina aitwa aleni,
sijampata kwa ndoto,kanipatia manani,
haikuwa wangu wito,sasa ninaye nyumbani,
Tumieni jina langu,na sio mama fulani
akijalia manani,wazazi zawadi kuu,
jina lako ni jamali,katu sipende makuu,
mtoto wako ni Ali,wewe baba ya Abuu,
Tumieni jina langu,na sio mama fulani
unabagua watoto,kutumia jina moja,
wewe ni mama Kizito,mumeo baba Mhoja,
wajiita mama wini,sisi watupa utata,
Tumieni jina langu,na sio mama fulani
watoto kuwabagua,ni dhambi kubwa kwa Mola,
jina moja wachagua,ndugu yangu Halahala,
baba John nakwambia,kamwambie na Hamala,
Tumieni jina langu,na sio mama fulani
Wednesday, September 14, 2011
ELIMU CHAI YA MOTO
Hapo kale tuliimba,elimu chai ya moto,
mashairi tulipamba,tuliyaimba kitoto,
mambo yaliyotukumba,leo hii kama ndoto
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
ukweli nimebaini,elimu kweli bahari,
kuandika vibaoni,hadi kwenye daftari,
unapofika shuleni,vingi unatahayari,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
waukumbuka umande,asubuhi na mapema,
wapata chai na kande,kasi huku ukihema,
gari wapi ukapande,wewe mtoto wa mama,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
hebu kumbuka walimu,walivyokuwa na wito,
asubuhi wajihimu,yale ni gani mapito,
hawakuwa warasimu,kufanya mambo mkato,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
wazikumbuka adhabu,zile walizozitoa,
zilikuwa na sababu,wala hawakukosea,
walitufunza adabu,na nidhamu kutopea,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
ulikuwa kama wimbo,lakini una maana,
haukuwa na mafumbo,wala beti kukinzana,
kichwani kama ulimbo,jinsi ulivyonatana,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
hebu kumbuka adhabu,kama kuchimba visiki,
ilikuwa kweli tabu,kama kuvunja kasiki,
yote yaliyonisibu,sasa yanipa riziki,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie
uji bila ya sukari,ilikuwa kawaida,
mfano sawa futari,bila asali si shida,
tebo tulivyokariri,kama mgonjwa na soda,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
ukifika sekondari,mambo yanabadilika,
sasa hakuna'habari',ung'eng'e kuutandika,
ilikuwa kweli heri,mambo yakaeleweka,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
huko elimu ya juu,mambo ni kizaazaa,
.hakuhitaji makuu,vingi utavishangaa,
hata walio wakuu,kule wengi wazubaa,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
ulichanganya'madesa',mambo yalipokutinga,
jambo lililokupasa,ni vizuri kujipanga,
hilo sana sio kosa,bali ulipoboronga,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
umeingia kazini,huko hakuna kudesa,
ulichopata chuoni,kifanyie kazi sasa,
ulifanya'magirini',sasa wapata mikasa,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
elimu chai ya moto,ukinywa upulizie,
ni sawa kupata kito,nani akakutunzie,
elimu kweli ni moto,lazima upulizie,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
sasa ninamalizia,ELIMU kweli ni mali,
jinsi unavyodhania,pia tumia akili,
sio cheti fumbatia,kama ilivyo hamali,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
mashairi tulipamba,tuliyaimba kitoto,
mambo yaliyotukumba,leo hii kama ndoto
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
ukweli nimebaini,elimu kweli bahari,
kuandika vibaoni,hadi kwenye daftari,
unapofika shuleni,vingi unatahayari,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
waukumbuka umande,asubuhi na mapema,
wapata chai na kande,kasi huku ukihema,
gari wapi ukapande,wewe mtoto wa mama,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
hebu kumbuka walimu,walivyokuwa na wito,
asubuhi wajihimu,yale ni gani mapito,
hawakuwa warasimu,kufanya mambo mkato,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
wazikumbuka adhabu,zile walizozitoa,
zilikuwa na sababu,wala hawakukosea,
walitufunza adabu,na nidhamu kutopea,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
ulikuwa kama wimbo,lakini una maana,
haukuwa na mafumbo,wala beti kukinzana,
kichwani kama ulimbo,jinsi ulivyonatana,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
hebu kumbuka adhabu,kama kuchimba visiki,
ilikuwa kweli tabu,kama kuvunja kasiki,
yote yaliyonisibu,sasa yanipa riziki,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie
uji bila ya sukari,ilikuwa kawaida,
mfano sawa futari,bila asali si shida,
tebo tulivyokariri,kama mgonjwa na soda,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
ukifika sekondari,mambo yanabadilika,
sasa hakuna'habari',ung'eng'e kuutandika,
ilikuwa kweli heri,mambo yakaeleweka,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
huko elimu ya juu,mambo ni kizaazaa,
.hakuhitaji makuu,vingi utavishangaa,
hata walio wakuu,kule wengi wazubaa,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
ulichanganya'madesa',mambo yalipokutinga,
jambo lililokupasa,ni vizuri kujipanga,
hilo sana sio kosa,bali ulipoboronga,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
umeingia kazini,huko hakuna kudesa,
ulichopata chuoni,kifanyie kazi sasa,
ulifanya'magirini',sasa wapata mikasa,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
elimu chai ya moto,ukinywa upulizie,
ni sawa kupata kito,nani akakutunzie,
elimu kweli ni moto,lazima upulizie,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
sasa ninamalizia,ELIMU kweli ni mali,
jinsi unavyodhania,pia tumia akili,
sio cheti fumbatia,kama ilivyo hamali,
Elimu chai ya moto,ukinywa upulizie.
UMARIDADI.
somo la umaridadi,wengi linatusumbua,
ninasema makusudi,tena nimekusudia,
kusema kwangu si budi,wote nitawaambia,
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
wengi twajipendekeza,tuonekanae kwa watu,
jinsi tunavyojikweza,kusema katu siwezi,
akili kuituliza,tokeni kwenye misitu,
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
wengine umaridadi,ni kuvaa suti safi,
chumbani wawashe udi,kuipata hewa safi,
watoto kwa makusudi,magodoro ni ya sufi,
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
kutwa unavaa tai,twakuona wapendeza,
wewe ni baba hufai,watu baki huwatunza,
nyumbani kwako hukai,watu baki wajikweza
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
michango mingi watoa,kila kamati hukosi,
majigambo wayatoa,kwa vikao vya harusi,
laki tatu unatoa,wewe huko ndiye bosi,
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
mama nawe washangaza,vitenge zamu kwa zamu
mtaani waongoza,watu imeisha hamu,
kanga nazo umejaza,watu wote twafahamu,
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
watoto nguo ni mbovu,mama atia huruma,
hebu uache uovu,baba jaribu kupima,
twaomba acha uovu,jaribu kuona nyuma,
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
mengi nimeyaongea,kuhusu umaridadi,,
haya sitawaonea,wafanyao makusudi,
huruma nawaonea,huo si umaridadi,
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
hapa mwisho nimefika,sana nimeongelea,
ujumbe ukikufika,ustarabu jongea,
sifa hovyo kujipaka,bure utaja umia
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
ninasema makusudi,tena nimekusudia,
kusema kwangu si budi,wote nitawaambia,
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
wengi twajipendekeza,tuonekanae kwa watu,
jinsi tunavyojikweza,kusema katu siwezi,
akili kuituliza,tokeni kwenye misitu,
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
wengine umaridadi,ni kuvaa suti safi,
chumbani wawashe udi,kuipata hewa safi,
watoto kwa makusudi,magodoro ni ya sufi,
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
kutwa unavaa tai,twakuona wapendeza,
wewe ni baba hufai,watu baki huwatunza,
nyumbani kwako hukai,watu baki wajikweza
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
michango mingi watoa,kila kamati hukosi,
majigambo wayatoa,kwa vikao vya harusi,
laki tatu unatoa,wewe huko ndiye bosi,
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
mama nawe washangaza,vitenge zamu kwa zamu
mtaani waongoza,watu imeisha hamu,
kanga nazo umejaza,watu wote twafahamu,
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
watoto nguo ni mbovu,mama atia huruma,
hebu uache uovu,baba jaribu kupima,
twaomba acha uovu,jaribu kuona nyuma,
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
mengi nimeyaongea,kuhusu umaridadi,,
haya sitawaonea,wafanyao makusudi,
huruma nawaonea,huo si umaridadi,
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
hapa mwisho nimefika,sana nimeongelea,
ujumbe ukikufika,ustarabu jongea,
sifa hovyo kujipaka,bure utaja umia
Umaridadi mzuri,ni kujali familia.
TUWAHESHIMU WAZAZI
wazazi Mungu wa pili,hili sote twalijua,
lazima wawe wawili,katika hii dunia,
wanapoishi mahali,ni Mola kawajalia
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika.
tulipokuwa wadogo,sana tulilalamika,
tulijifanya ni mbogo,chakula kihitajika,
hatukutaka muhogo,moyo haukuridhia,
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika.
kulea kazi ya baba,hakika pia ya mama,
kuwalea kwa mahaba,ulezi si lelemama,
kama chakula ni haba,wazazi walijinyima,
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika.
walitupeleka shule,mambo mengi waliacha,
kwa pesa yao kichele,anasa waliziacha,
kwenda huku hata kule,walishindia mchicha,
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika.
uwezo waliopata,ndio waliotumia,
kidogo walichopata,ndicho walitupatia,
na pesa sio karata,dume ukajilambia,
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika.
kuwalaumu si haki,jaribu kufikiria,
hebu acha kuhamaki,maisha jifikiria,
tena uache dhihaki,wazazi luwarushia,
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika.
elimu waliyokupa,uitumie vizuri,
ulianza kaa hapa,maisha ukivinjari,
sasa nini unaapa,wazazi hawafikiri,
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika.
hivi sasa umeoa,una mkeo nyumbani,
ilani sasa watoa,huwataki asilani,
mahari waliyotoa,hukumbuki abadani,
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika
nitaongea mangapi,yote mbona mwaelewa,
busara nitoe wapi,wazazi wanaelewa,
mhariri toa kopi,watu wapate elewa,
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika.
lazima wawe wawili,katika hii dunia,
wanapoishi mahali,ni Mola kawajalia
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika.
tulipokuwa wadogo,sana tulilalamika,
tulijifanya ni mbogo,chakula kihitajika,
hatukutaka muhogo,moyo haukuridhia,
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika.
kulea kazi ya baba,hakika pia ya mama,
kuwalea kwa mahaba,ulezi si lelemama,
kama chakula ni haba,wazazi walijinyima,
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika.
walitupeleka shule,mambo mengi waliacha,
kwa pesa yao kichele,anasa waliziacha,
kwenda huku hata kule,walishindia mchicha,
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika.
uwezo waliopata,ndio waliotumia,
kidogo walichopata,ndicho walitupatia,
na pesa sio karata,dume ukajilambia,
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika.
kuwalaumu si haki,jaribu kufikiria,
hebu acha kuhamaki,maisha jifikiria,
tena uache dhihaki,wazazi luwarushia,
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika.
elimu waliyokupa,uitumie vizuri,
ulianza kaa hapa,maisha ukivinjari,
sasa nini unaapa,wazazi hawafikiri,
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika.
hivi sasa umeoa,una mkeo nyumbani,
ilani sasa watoa,huwataki asilani,
mahari waliyotoa,hukumbuki abadani,
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika
nitaongea mangapi,yote mbona mwaelewa,
busara nitoe wapi,wazazi wanaelewa,
mhariri toa kopi,watu wapate elewa,
Tuwaheshimu wazazi,sana wamehangaika.
TUELEZANE UKWELI
utnzi ni kazi ngumu,japo tunaitamani,
kupanga beti vigumu,tena ziwe na thamani,
upatapo jambo gumu,lisumbue akilini,
Tuelezane ukweli kama kweli twapendana.
nikuonapo yakini,moyo wangu hupasuka,
binti uliye makini,tena ulivyoumbika,
mimi nitafanya nini,kutwa ninaweweseka,
Tuelezane ukweli kama kweli twapendana.
mara nyingi nimewaza,nikwambie kitu gani,
huenda utapuuza,kuniona hayawani,
jibu safi lanipoza,kama maji mtungini,
Tuelezane ukweli kama kweli twapendana.
mengi ya kusema sina,ushairi siujui,
naomba jibu mwanana,jeupe mfano tui,
usinione wa jana,au ni mtu sifai,
Tuelezane ukweli kama kweli twapendana.
kupanga beti vigumu,tena ziwe na thamani,
upatapo jambo gumu,lisumbue akilini,
Tuelezane ukweli kama kweli twapendana.
nikuonapo yakini,moyo wangu hupasuka,
binti uliye makini,tena ulivyoumbika,
mimi nitafanya nini,kutwa ninaweweseka,
Tuelezane ukweli kama kweli twapendana.
mara nyingi nimewaza,nikwambie kitu gani,
huenda utapuuza,kuniona hayawani,
jibu safi lanipoza,kama maji mtungini,
Tuelezane ukweli kama kweli twapendana.
mengi ya kusema sina,ushairi siujui,
naomba jibu mwanana,jeupe mfano tui,
usinione wa jana,au ni mtu sifai,
Tuelezane ukweli kama kweli twapendana.
Thursday, September 8, 2011
TUACHE TABIA MBAYA
tabia mbaya ni nyingi,ni sawa wingi wa watu,
nitayaongea mengi,aibu sioni katu,
nimeona watu wengi,roho zimejaa kutu,
tuache tabia mbaya,duniani tupendane.
mara nyingi nimeona,mambo ya kusikitisha,
matajiri wajiona,sana inaogopesha,
fukara wakituona,magari tope yarusha
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
wafika nyumbani kwangu,kuja kunitembelea,
nakuona ndugu yangu,upendo twajijengea,
ninapokaa si pangu,mimi nimejipangia
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
umekaa sebuleni,macho macho yako pekupeku,
wachungulia chumbani,nini uliacha huku,
si vizuri asilani,wewe sio panya buku,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
mezani kuna barua,nimeandikiwa mimi,
bado sijaifungua,imetoka kwa Msami,
wewe unaichukua,unajitia msomi,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
jambo hili la barua,sana linanichukiza,
leo hii naamua,nilitoe kwenye giza,
kama umeifungua,uijibu nakweleza,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
nitayaongea mengi,aibu sioni katu,
nimeona watu wengi,roho zimejaa kutu,
tuache tabia mbaya,duniani tupendane.
mara nyingi nimeona,mambo ya kusikitisha,
matajiri wajiona,sana inaogopesha,
fukara wakituona,magari tope yarusha
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
wafika nyumbani kwangu,kuja kunitembelea,
nakuona ndugu yangu,upendo twajijengea,
ninapokaa si pangu,mimi nimejipangia
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
umekaa sebuleni,macho macho yako pekupeku,
wachungulia chumbani,nini uliacha huku,
si vizuri asilani,wewe sio panya buku,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
mezani kuna barua,nimeandikiwa mimi,
bado sijaifungua,imetoka kwa Msami,
wewe unaichukua,unajitia msomi,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
jambo hili la barua,sana linanichukiza,
leo hii naamua,nilitoe kwenye giza,
kama umeifungua,uijibu nakweleza,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
SHIDA HAINA ADABU.
kila mtu ana shida,ingawa hazifanani,
shida haijali muda,wala una kazi gani,
shida ni sawa husuda,hivi leo ninaghani,
shida haina adabu,jamani nawaeleza.
shida inapokupata,sana unahangaika,
pumzi utaivuta,na jasho litakutoka,
majonzi yatafuata,mwili ukatetemeka,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
shida inapokupata.waweza omba mkopo,
upunguze furukuta,mfano ule wa popo,
lipa deni kulifuta,ulikopa kwa kiapo,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
wengi tunawashangaa,shida inapowapata,
waja kwa kunyenyekea,tena mwendo wa kunyata,
shida wakielezea,huruma inakupata,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
nisemayo ni hakika,jaribu kujiuliza,
kama halijakufika,sasa ninakueleza,
akilini lifutika,wasije wakakuliza,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
ahadi kweli ni deni,ukikopa kweli lipa,
usiufanye uhuni,kwa imani alikupa
sasa vipi wamuhini,hutaki deni kulipa,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
shida haijali muda,wala una kazi gani,
shida ni sawa husuda,hivi leo ninaghani,
shida haina adabu,jamani nawaeleza.
shida inapokupata,sana unahangaika,
pumzi utaivuta,na jasho litakutoka,
majonzi yatafuata,mwili ukatetemeka,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
shida inapokupata.waweza omba mkopo,
upunguze furukuta,mfano ule wa popo,
lipa deni kulifuta,ulikopa kwa kiapo,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
wengi tunawashangaa,shida inapowapata,
waja kwa kunyenyekea,tena mwendo wa kunyata,
shida wakielezea,huruma inakupata,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
nisemayo ni hakika,jaribu kujiuliza,
kama halijakufika,sasa ninakueleza,
akilini lifutika,wasije wakakuliza,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
ahadi kweli ni deni,ukikopa kweli lipa,
usiufanye uhuni,kwa imani alikupa
sasa vipi wamuhini,hutaki deni kulipa,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
JAHAZI LAENDA KOMBO
sisi sote wasafiri,safari yetu ni moja,
tulianza adhuhuri,kwa kuujenga umoja,
jambo tulilofikiri,tulifikiri pamoja,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
kuivinjari bahari,unahitaji ujuzi,
nahodha awe mahiri,kuvikwepa vizuizi,
afikirie vizuri,tusipate pingamizi,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
hata sisi wasafiri,busara tunahitaji
kazi iwe tafakari,na kumuomba mpaji,
tusiwe kama kafiri,tumuombe Muumbaji,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
nahodha tunakuomba,safari iwe makini,
sio kwamba twajikomba,tukafike kisiwani,
wasafiri tunaomba,tuongoze kwa makini,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
unahodha kazi ngumu,katu sitoiamini
kuliongoza vigumu,kundi ndani jahazini,
waweza pata wazimu,kama ng'ombe machinjoni,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
wapi yu msaidizi,kupokea ukichoka,
tumepigwa bumbuazi,wenzetu watatucheka,
nahodha hukumaizi,mwenzio ana vibweka,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
kitambo kimeshapita,bado hatujielewi,
njia ipi tumepita,mbona safari haiwi,
hatukuweza kupata,hata harufu ya Wawi,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
dhoruba imetukumba,ubavu umetoboka
wewe bado unatamba,jahazi litaboreka,
abiria twakuomba,punguza vyako vibweka,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
sasa nini tunafanya,kweli twaanza kuzama,
tunafanana na panya,anayehaha kuhama,
awali tulikukanya,sasa waanza lalama,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
hapa mwisho nimefika,bado ninasononeka,
maafa yatatufika,hatuwezi nusurika,
mwisho hatutaufika,majini tutajizika,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
tulianza adhuhuri,kwa kuujenga umoja,
jambo tulilofikiri,tulifikiri pamoja,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
kuivinjari bahari,unahitaji ujuzi,
nahodha awe mahiri,kuvikwepa vizuizi,
afikirie vizuri,tusipate pingamizi,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
hata sisi wasafiri,busara tunahitaji
kazi iwe tafakari,na kumuomba mpaji,
tusiwe kama kafiri,tumuombe Muumbaji,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
nahodha tunakuomba,safari iwe makini,
sio kwamba twajikomba,tukafike kisiwani,
wasafiri tunaomba,tuongoze kwa makini,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
unahodha kazi ngumu,katu sitoiamini
kuliongoza vigumu,kundi ndani jahazini,
waweza pata wazimu,kama ng'ombe machinjoni,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
wapi yu msaidizi,kupokea ukichoka,
tumepigwa bumbuazi,wenzetu watatucheka,
nahodha hukumaizi,mwenzio ana vibweka,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
kitambo kimeshapita,bado hatujielewi,
njia ipi tumepita,mbona safari haiwi,
hatukuweza kupata,hata harufu ya Wawi,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
dhoruba imetukumba,ubavu umetoboka
wewe bado unatamba,jahazi litaboreka,
abiria twakuomba,punguza vyako vibweka,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
sasa nini tunafanya,kweli twaanza kuzama,
tunafanana na panya,anayehaha kuhama,
awali tulikukanya,sasa waanza lalama,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
hapa mwisho nimefika,bado ninasononeka,
maafa yatatufika,hatuwezi nusurika,
mwisho hatutaufika,majini tutajizika,
Jahazi laenda kombo,naogopa tutazama.
Wednesday, September 7, 2011
CHAKULANI WANISIMANGA.
kila atamani japo apate chakula,
njaa kweli si utani,kwa nini Mola kaumba,
sijaona asilani,kuishi bila ya kula,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
uhai ni wa thamani,nawe pia unajua,
maisha sio samani,tuache mchwa bangua,
ukipata cha makini,afya utajijengea,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
wasema nina tamaa,kisa ninataka kula,
uchu mimi umejaa,hiki ni chetu chakula,
simanzi imenikaa,ataniokoa Mola,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
chakula kilipotengwa,ulivamia kwa pupa,
sasa imekuwa nongwa,nami hapo kujitupa,
ulafi ulivyosongwa,wala waacha mifupa,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
nakumbuka zama hizo,mimi bado kuzaliwa,
hukwenda hata likizo,ukitwange sawasawa,
uliyofanya uozo,katu hukusingiziwa,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
unaniita mlafi,kisa nami nakitaka,
hata nipigwe makofi,sikubali nitafika
wewe kweli si msafi,wanawa kwa maji taka,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
wanitangaza kwa watu,eti mimi vuvuzela,
nami sikubali katu,hapo wote tutakula,
hata nipigwe viatu,tutakutana mahala,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
kila siku wala wewe,leo niachie mimi,
vipi wapata kiwewe,ulishapata uchumi,
wataka nipiga mawe,umekujaa umimi,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
kichekesho umetoa eti sina uzoefu,
hebu nenda angalia,jinsi alivyo siafu,
jinsi anavyojitoa,tena moyo mkunjufu,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe
muda wako umeisha,ulianza zama zile,
inakupasa kupisha,tena bila makelele,
chakula kimekutosha,na wana waache wale,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
njaa kweli si utani,kwa nini Mola kaumba,
sijaona asilani,kuishi bila ya kula,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
uhai ni wa thamani,nawe pia unajua,
maisha sio samani,tuache mchwa bangua,
ukipata cha makini,afya utajijengea,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
wasema nina tamaa,kisa ninataka kula,
uchu mimi umejaa,hiki ni chetu chakula,
simanzi imenikaa,ataniokoa Mola,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
chakula kilipotengwa,ulivamia kwa pupa,
sasa imekuwa nongwa,nami hapo kujitupa,
ulafi ulivyosongwa,wala waacha mifupa,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
nakumbuka zama hizo,mimi bado kuzaliwa,
hukwenda hata likizo,ukitwange sawasawa,
uliyofanya uozo,katu hukusingiziwa,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
unaniita mlafi,kisa nami nakitaka,
hata nipigwe makofi,sikubali nitafika
wewe kweli si msafi,wanawa kwa maji taka,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
wanitangaza kwa watu,eti mimi vuvuzela,
nami sikubali katu,hapo wote tutakula,
hata nipigwe viatu,tutakutana mahala,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
kila siku wala wewe,leo niachie mimi,
vipi wapata kiwewe,ulishapata uchumi,
wataka nipiga mawe,umekujaa umimi,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
kichekesho umetoa eti sina uzoefu,
hebu nenda angalia,jinsi alivyo siafu,
jinsi anavyojitoa,tena moyo mkunjufu,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe
muda wako umeisha,ulianza zama zile,
inakupasa kupisha,tena bila makelele,
chakula kimekutosha,na wana waache wale,
Vipi unanisimanga,kula ulianza wewe.
KICHEKO
mwenzako anapotingwa,nini kinakuchekesha,
hata kama ni mfungwa,maombi yapasa kesha,
mwenzako anaponyongwa,nini chakufurahisha,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka.
pesa mfukoni hana,wewe unachekelea,
unaanza kumkana,kipi unafurahia,
una raha kumuona,kutwa akunyenyekea,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
nimefeli mtihani,wewe unafurahia,
nimeshindwa kwenye fani,sherehe wajifanyia,
nimefukuzwa kazini,wasema uliyajua,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
maombi bila majibu,yangu unachekelea,
kitu kipi cha ajabu,majibu ukisikia,
hiyo isiwe sababu,mimi nitasubiria,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
mume wangu kanibwaga,wewe unachekelea,
kisa eti hakuaga,wadhani kanikimbia,
wahi nyumbani kuoga,fitina umezoea,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
mke wangu kaondoka,wewe unafurahia,
machozi yakudondoka,vile ukichekelea,
ndoa yetu kuvunjika,wapweke tutabakia,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
tukianza rudiana,wewe kwako ni msiba,
pembeni unajibana,majungu yako si haba,
amani kupatikana,japo katika kibaba,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
kicheko kile halali,wewe kwako haucheki,
huzuni kila mahali,watu wote wakucheki,
furaha kwako muhali,umebaki kuhamaki,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
cheka kicheko cha heri,tufurahi kwa pamoja,
sio kucheka pa shari,utavuruga umoja,
nakupasha kishairi,tazama hilo daraja,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
beti kumi zinatosha,nyingi bure utachoka,
hayo niliyokupasha,moyoni hebu futika,
acha kujibabaisha,busara itakutoka,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
hata kama ni mfungwa,maombi yapasa kesha,
mwenzako anaponyongwa,nini chakufurahisha,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka.
pesa mfukoni hana,wewe unachekelea,
unaanza kumkana,kipi unafurahia,
una raha kumuona,kutwa akunyenyekea,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
nimefeli mtihani,wewe unafurahia,
nimeshindwa kwenye fani,sherehe wajifanyia,
nimefukuzwa kazini,wasema uliyajua,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
maombi bila majibu,yangu unachekelea,
kitu kipi cha ajabu,majibu ukisikia,
hiyo isiwe sababu,mimi nitasubiria,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
mume wangu kanibwaga,wewe unachekelea,
kisa eti hakuaga,wadhani kanikimbia,
wahi nyumbani kuoga,fitina umezoea,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
mke wangu kaondoka,wewe unafurahia,
machozi yakudondoka,vile ukichekelea,
ndoa yetu kuvunjika,wapweke tutabakia,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
tukianza rudiana,wewe kwako ni msiba,
pembeni unajibana,majungu yako si haba,
amani kupatikana,japo katika kibaba,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
kicheko kile halali,wewe kwako haucheki,
huzuni kila mahali,watu wote wakucheki,
furaha kwako muhali,umebaki kuhamaki,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
cheka kicheko cha heri,tufurahi kwa pamoja,
sio kucheka pa shari,utavuruga umoja,
nakupasha kishairi,tazama hilo daraja,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
beti kumi zinatosha,nyingi bure utachoka,
hayo niliyokupasha,moyoni hebu futika,
acha kujibabaisha,busara itakutoka,
Hivyo vyote ni vicheko,mengine si ya kucheka
Tuesday, September 6, 2011
KUOA KITU KIZURI,HATA KUOLEWA PIA
kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia,
kupata mke mzuri,hakika inavutia,
usioe wa kiburi,utakuja jijutia,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
hata wewe mwanamke,chagua mume makini,
usipate wa makeke,kamwe hatolala ndani,
kutwa mshikemshike,kutotulia nyumbani,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
huyo uliyechagua,umechagua vizuri,
sana uliangalia,akakutia kiwewe,
sasa nini unalia,suluhisheni wenyewe,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
mnapokorofishana,budi itaneni ndani,
ni lazima kupishana,na huyo wako mwandani,
kwa koo mmepishana,hata kwa ndani rohoni,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
mara nyingi nashangaa,watu wanapogombana,
miaka mingi wamekaa,maisha yao mwanana,
watoto wamewazaa,tena wanaofanana,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
waume wanishangaza,msimamo wao duni,
siri zao watangaza,na mambo yao ya ndani
wameshindwa kuongoza,wanatanga mitaani,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
nawe mke wachekesha,jambo linapokufika,
usiku kucha wakesha,sana unahangaika,
usije moto kuwasha,maafa yatawafika,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
mambo yenu ya nyumbani,malizieni nyumbani,
si wazazi aslilani,katu hawatobaini,
kuwasumbua si shani,mtawapa tafrani,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
mume mbio kwa wazazi,tatizo likitokea,
na mke bila ajizi,kwao enda simulia,
utafuteni mzizi,wa tatizo kutatua,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
haya ni yangu mawazo,si jambo nasimulia,
isije leta mzozo,kwa walioyatukia,
ndoa mbovu ni uozo,hakika nawaambia
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
kupata mke mzuri,hakika inavutia,
usioe wa kiburi,utakuja jijutia,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
hata wewe mwanamke,chagua mume makini,
usipate wa makeke,kamwe hatolala ndani,
kutwa mshikemshike,kutotulia nyumbani,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
huyo uliyechagua,umechagua vizuri,
sana uliangalia,akakutia kiwewe,
sasa nini unalia,suluhisheni wenyewe,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
mnapokorofishana,budi itaneni ndani,
ni lazima kupishana,na huyo wako mwandani,
kwa koo mmepishana,hata kwa ndani rohoni,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
mara nyingi nashangaa,watu wanapogombana,
miaka mingi wamekaa,maisha yao mwanana,
watoto wamewazaa,tena wanaofanana,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
waume wanishangaza,msimamo wao duni,
siri zao watangaza,na mambo yao ya ndani
wameshindwa kuongoza,wanatanga mitaani,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
nawe mke wachekesha,jambo linapokufika,
usiku kucha wakesha,sana unahangaika,
usije moto kuwasha,maafa yatawafika,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
mambo yenu ya nyumbani,malizieni nyumbani,
si wazazi aslilani,katu hawatobaini,
kuwasumbua si shani,mtawapa tafrani,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
mume mbio kwa wazazi,tatizo likitokea,
na mke bila ajizi,kwao enda simulia,
utafuteni mzizi,wa tatizo kutatua,
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
haya ni yangu mawazo,si jambo nasimulia,
isije leta mzozo,kwa walioyatukia,
ndoa mbovu ni uozo,hakika nawaambia
Kuoa kitu kizuri,hata kuolewa pia.
KILA KITU KINA JINA
kila mtu ana jina,hata kama yafanana,
kila kitu kina jina,kuweka vitu bayana,
kila mnyama kwa jina,hata kama wafanana,
kila kitu kina jina,kuweka mambo bayana.
mi sijapata kuona,kitu kisicho na jina,
mitindo nguo twashona,yote yapewa majina,
magari unayaona,ya starehe mwanana,
kila kitu kina jina,kuweka mambo bayana.
hata kama twafanana,tabia zitofanana,
nyuso zetu zote pana,kweli twafanana sana,
yachunguze kwa mapana,yote ajua Rabana,
kila kitu kina jina,kuweka mambo bayana.
majina tunapeana,mwingine aitwa Ana,
majina si kufaana,hilo halina maana,
jina baya mi nakana,nipate janga kupona,
kila kitu kina jina,kuweka mambo bayana.
wewe Vumi msichana,yeye Juma mvulana,
nywele vipi mwasukana,jinsia mmepishana,
saluni mwasukumana,tabia hiyo nakana,
kila kitu kina jina,kuweka mambo bayana.
wavulana wapeana,vitu kama wasichana,
sketi zinawabana,huku wao wavulana,
watembea kisichana,kwapani pochi wabana,
kila kitu kina jina,kuweka mambo bayana.
tukuite lipi jina,tabia zimepishana,
jinsi tunavyokuona,umbo lako si bayana,
sauti unaibana,mwendo wako kisichana,
kila kitu kina jina,kuweka mambo bayana.
Mola hayo anaona,siku moja takutana,
heleni zivojishona,pete nazo kila kona,
kinyaa mimi naona,kila siku na sonona,
kila kitu kina jina,kuweka mambo bayana.
kila kitu kina jina,kuweka vitu bayana,
kila mnyama kwa jina,hata kama wafanana,
kila kitu kina jina,kuweka mambo bayana.
mi sijapata kuona,kitu kisicho na jina,
mitindo nguo twashona,yote yapewa majina,
magari unayaona,ya starehe mwanana,
kila kitu kina jina,kuweka mambo bayana.
hata kama twafanana,tabia zitofanana,
nyuso zetu zote pana,kweli twafanana sana,
yachunguze kwa mapana,yote ajua Rabana,
kila kitu kina jina,kuweka mambo bayana.
majina tunapeana,mwingine aitwa Ana,
majina si kufaana,hilo halina maana,
jina baya mi nakana,nipate janga kupona,
kila kitu kina jina,kuweka mambo bayana.
wewe Vumi msichana,yeye Juma mvulana,
nywele vipi mwasukana,jinsia mmepishana,
saluni mwasukumana,tabia hiyo nakana,
kila kitu kina jina,kuweka mambo bayana.
wavulana wapeana,vitu kama wasichana,
sketi zinawabana,huku wao wavulana,
watembea kisichana,kwapani pochi wabana,
kila kitu kina jina,kuweka mambo bayana.
tukuite lipi jina,tabia zimepishana,
jinsi tunavyokuona,umbo lako si bayana,
sauti unaibana,mwendo wako kisichana,
kila kitu kina jina,kuweka mambo bayana.
Mola hayo anaona,siku moja takutana,
heleni zivojishona,pete nazo kila kona,
kinyaa mimi naona,kila siku na sonona,
kila kitu kina jina,kuweka mambo bayana.
OFISI
ofisi hiyo si yako,umepewa ni dhamana,
mgeni kafika kwako,usimpime kwa dhana,
kumbuka yako miiko,sikiliza kwa mapana,
ewe bosi twakuomba,uwathamini wageni.
mgeni kafika kwako,wewe uko wimawima,
hajaja nyumbani kwako,kaja ofisi ya umma,
ofisi si chumba chako,ikumbuke yako dhima,
ewe bosi twakuomba,uwathamini wageni.
yupi utamthamini,aje amevaa suti,
au yule wa vimini,viatu kama mabuti,
siku utaja amini,kitumbua si chapati,
ewe bosi twakuomba,uwathamini wageni.
wageni wote ni sawa,bila kutazama hali,
sio kumjali Hawa,Konisaga hana mali,
Vita mwana wa Kawawa,Robert Msakamali,
ewe bosi twakuomba,uwathamini wageni.
mgeni kafika kwako,usimpime kwa dhana,
kumbuka yako miiko,sikiliza kwa mapana,
ewe bosi twakuomba,uwathamini wageni.
mgeni kafika kwako,wewe uko wimawima,
hajaja nyumbani kwako,kaja ofisi ya umma,
ofisi si chumba chako,ikumbuke yako dhima,
ewe bosi twakuomba,uwathamini wageni.
yupi utamthamini,aje amevaa suti,
au yule wa vimini,viatu kama mabuti,
siku utaja amini,kitumbua si chapati,
ewe bosi twakuomba,uwathamini wageni.
wageni wote ni sawa,bila kutazama hali,
sio kumjali Hawa,Konisaga hana mali,
Vita mwana wa Kawawa,Robert Msakamali,
ewe bosi twakuomba,uwathamini wageni.
KARAMU TUNAZIPENDA
wengi twapenda karamu,twazisubiri kwa hamu,
kama hili hufahamu,jibu utapata humu,
utavipata vitamu,kamwe hutapata sumu,
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
nilichukua kalamu,kueleza umuhimu,
ninataka kufahamu,japo katika awamu,
karamu sio swaumu,kupata si jambo gumu,.
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
karamu nyingi fahamu,zaweza kuleta pumu,
jinsi tunavyozifomu,nyingizo sio muhimu
kuzijua nina hamu,moyo pate tabasamu
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
mimi ninavyofahamu,karamu si marhamu,
imeshaniisha hamu,nitamwuliza mwalimu,
vipi hizo zinadumu,tena daima dawamu,
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
unajilipua bomu,tena huku wafahamu,
hiyo kwako ni karamu,kweli huna ufahamu,
ulitumia vidumu,kuliunda hilo bomu,
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
wanipatia salamu,moyoni huna fahamu,
waanza kumwaga sumu,ofisini nisidumu,
umekuwa ni hasimu,kama unavuta'ndumu'
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
ndoa yangu haidumu,unajifanya hakimu,
asubuhi wajihimu,unaleta uhasimu,
kwetu wewe si Rahimu,ndoa yetu itadumu,
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
ninapenda ufahamu,sitaki ugomvi humu,
wapi ulikohitimu,feki wako ualimu,
unatushusha stimu,nenda zako jehanamu
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
kama hili hufahamu,jibu utapata humu,
utavipata vitamu,kamwe hutapata sumu,
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
nilichukua kalamu,kueleza umuhimu,
ninataka kufahamu,japo katika awamu,
karamu sio swaumu,kupata si jambo gumu,.
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
karamu nyingi fahamu,zaweza kuleta pumu,
jinsi tunavyozifomu,nyingizo sio muhimu
kuzijua nina hamu,moyo pate tabasamu
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
mimi ninavyofahamu,karamu si marhamu,
imeshaniisha hamu,nitamwuliza mwalimu,
vipi hizo zinadumu,tena daima dawamu,
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
unajilipua bomu,tena huku wafahamu,
hiyo kwako ni karamu,kweli huna ufahamu,
ulitumia vidumu,kuliunda hilo bomu,
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
wanipatia salamu,moyoni huna fahamu,
waanza kumwaga sumu,ofisini nisidumu,
umekuwa ni hasimu,kama unavuta'ndumu'
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
ndoa yangu haidumu,unajifanya hakimu,
asubuhi wajihimu,unaleta uhasimu,
kwetu wewe si Rahimu,ndoa yetu itadumu,
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
ninapenda ufahamu,sitaki ugomvi humu,
wapi ulikohitimu,feki wako ualimu,
unatushusha stimu,nenda zako jehanamu
karamu tunazipenda,nyingi zake si sahihi
CHETI CHA NDOA.
Vyeti vyote twavijua,toka vyuo mbalimbali,
hata ukivichungua,hakika utakubali,
jambo ninaloshangaa,vyeti vingi si vya kweli,
Cheti hiki unapewa,bila ya kwenda chuoni.
Cheti hiki mnatoa,sijaona diploma,
wasomi nawashangaa,mwakipokea kwa dhima,
tena mwakichekelea,kwa heshima taadhima,
wewe una digrii,cheti wapata cha nini
wapi niliposomea,mnanipatia cheti,
sana hili nashangaa,hoja namwaga kwa beti,
cheti mnanipatia,kweli kitaleta shoti,
Cheti bila mtihani,sijaona asilani.
hata kusoma sijui,ninakariri majibu,
fumbo hili halifai,mengi yataja nisibu,
siri ya ndani hujui,ni nini chakughiribu,
majibu tunakariri,watu wanashangilia
nimempenda Mwasiti,ndoa tunaitangaza,
shehe aja anaketi,aanza kuwauliza,
jama kipo kizuizi,watu hawa nawaoza,
Chuo gani tulikwenda,mnatupatia cheti.
Koni wampenda pendo,ndio baba Askofu,
sasa tunaanza mwendo,mambo yetu manyoofu,
kila mtu ana windo,na mioyo mikunjufu,
mchezo wa kuigiza,cheti hicho unapewa
chuo cha ndoa ki wapi,mimi nipate somea,
majibu wote twakopi,cheti bila kusomea,
vyeti hivyo kama pipi,sisi mnatugawia,
cheti hicho sikitaki,sana chaleta majuto.
kichekesho maprofesa,nao wanakipokea,
ni wapi walipodesa,chuo walikopitia,
ujinga unawatesa,mkumbo watumbukia,
wasomi wanapata cheti,bila kusoma chuoni.
wengine mbio bomani,ndoa kwenda ifungia,
nayo katu sitamani,balaa najizulia,
cheti bila ya chuoni,uchuro twajizolea,
wote wenye vyote hivyo,hakika nawashangaa.
kashangae kanisani,nderemo vigelegele,
wachumba wanasaini,mwanzo wa ngoma ni lele,
sijaona maishani,kitu mfano wa kile,
usinishangae mimi,kashangae hicho cheti.
viwango hawatakidhi,vyeti hivyo ni balaa,
jinsi vinavyoniudhi,wengine wajivunia,
vyeti hivyo ni maradhi,ya moyo jitafutia,
hicho kinaitwa cheti,diploma iko wapi
kama hujajiuliza,hebu anza jishangaa,
si kwamba nakipuuza,heshima nakitunzia,
sifa tulivyokijaza,watu wakifukuzia,
sote twakijua cheti,digrii iko wapi?
najua nitawakwaza,maoni yangu kutoa,
hebu jaribu kuwaza,chuo gani wanatoa,
cheti sitakipuuza,wote mmekiridhia,
dole gumba linatosha,kupata cheti cha ndoa.
kakague vyeti vyote,saini yako hukuti,
kwenye mikataba yote,kuwepo hiyo shuruti,
vyeti vya ndoa kalete,havielezi wakati,
jambo hili lichunguze,vyeti vingi tunafoji.
beti nyingi zinachosha,wengi zinawachukiza,
katu siwezi jikosha,sipendi kuwachokoza,
beti nilizozishusha,sio lengo kuwakwaza,
kama wakijua chuo,niambie nikasome.
wote
.
hata ukivichungua,hakika utakubali,
jambo ninaloshangaa,vyeti vingi si vya kweli,
Cheti hiki unapewa,bila ya kwenda chuoni.
Cheti hiki mnatoa,sijaona diploma,
wasomi nawashangaa,mwakipokea kwa dhima,
tena mwakichekelea,kwa heshima taadhima,
wewe una digrii,cheti wapata cha nini
wapi niliposomea,mnanipatia cheti,
sana hili nashangaa,hoja namwaga kwa beti,
cheti mnanipatia,kweli kitaleta shoti,
Cheti bila mtihani,sijaona asilani.
hata kusoma sijui,ninakariri majibu,
fumbo hili halifai,mengi yataja nisibu,
siri ya ndani hujui,ni nini chakughiribu,
majibu tunakariri,watu wanashangilia
nimempenda Mwasiti,ndoa tunaitangaza,
shehe aja anaketi,aanza kuwauliza,
jama kipo kizuizi,watu hawa nawaoza,
Chuo gani tulikwenda,mnatupatia cheti.
Koni wampenda pendo,ndio baba Askofu,
sasa tunaanza mwendo,mambo yetu manyoofu,
kila mtu ana windo,na mioyo mikunjufu,
mchezo wa kuigiza,cheti hicho unapewa
chuo cha ndoa ki wapi,mimi nipate somea,
majibu wote twakopi,cheti bila kusomea,
vyeti hivyo kama pipi,sisi mnatugawia,
cheti hicho sikitaki,sana chaleta majuto.
kichekesho maprofesa,nao wanakipokea,
ni wapi walipodesa,chuo walikopitia,
ujinga unawatesa,mkumbo watumbukia,
wasomi wanapata cheti,bila kusoma chuoni.
wengine mbio bomani,ndoa kwenda ifungia,
nayo katu sitamani,balaa najizulia,
cheti bila ya chuoni,uchuro twajizolea,
wote wenye vyote hivyo,hakika nawashangaa.
kashangae kanisani,nderemo vigelegele,
wachumba wanasaini,mwanzo wa ngoma ni lele,
sijaona maishani,kitu mfano wa kile,
usinishangae mimi,kashangae hicho cheti.
viwango hawatakidhi,vyeti hivyo ni balaa,
jinsi vinavyoniudhi,wengine wajivunia,
vyeti hivyo ni maradhi,ya moyo jitafutia,
hicho kinaitwa cheti,diploma iko wapi
kama hujajiuliza,hebu anza jishangaa,
si kwamba nakipuuza,heshima nakitunzia,
sifa tulivyokijaza,watu wakifukuzia,
sote twakijua cheti,digrii iko wapi?
najua nitawakwaza,maoni yangu kutoa,
hebu jaribu kuwaza,chuo gani wanatoa,
cheti sitakipuuza,wote mmekiridhia,
dole gumba linatosha,kupata cheti cha ndoa.
kakague vyeti vyote,saini yako hukuti,
kwenye mikataba yote,kuwepo hiyo shuruti,
vyeti vya ndoa kalete,havielezi wakati,
jambo hili lichunguze,vyeti vingi tunafoji.
beti nyingi zinachosha,wengi zinawachukiza,
katu siwezi jikosha,sipendi kuwachokoza,
beti nilizozishusha,sio lengo kuwakwaza,
kama wakijua chuo,niambie nikasome.
wote
.
HIZO SIO MILA POTOFU.
Hili wengi watacheka,nikianza simulia,
katu sifanyi vibweka,wazi nitaelezea,
mila zilivyotutoka,hatuna uasilia,
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka.
Kwenye jambo la kuoa,wazazi walilijua,
sisi twajiamulia,wachumba jichagulia,
kule kwao hujajua,uchumba jitangazia,
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka.
Huyo mke ulooa,wala kwao hupajui,
naye aliyekuoa,kesho atakukinai,
sababu usije zua,mila zao huzijui,
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka
Magonjwa unayajua,kutaja yote siwezi,
zipo koo za vichaa,zingine za wadokozi,
lipi unaloshangaa,wengine ni wachochezi
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka.
Lugha ile ya mafumbo,wazee walitumia,
hawakutumia fimbo,ujumbe kutupatia,
sasa vya nini vikumbo,tulia fuatilia,
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka
Kwa mama wajawazito,kula mayai ni mwiko,
huu ulikuwa wito,kumbuka sayansi yako,
usiwaze kwa mkato,ulikuwa kweli mwiko,
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka.
Zikumbuke enzi hizo,hospitali za shida,
kujifungua tatizo,tena kwachukua muda,
toto linene katizo,hili jibu sio mada,
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka.
Hebu fanya uchunguzi,ndoa zile za zamani,
hawakuwa wapuuzi,wala ndani tafrani,
hizi ndoa siku hizi,ni kama tuko vitani
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka.
Watoto wako wavivu,nini unachoshangaa,
umeshalipata kovu,katu huwezi litoa,
hata kama kwa mabavu,umeshaingia doa,
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka
Beti kumi zinatosha,sasa nikapumzike,
hata kama zinachusha,ziweke mahali pake,
usasa umenichosha,ndoa zetu sekeseke
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka.
katu sifanyi vibweka,wazi nitaelezea,
mila zilivyotutoka,hatuna uasilia,
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka.
Kwenye jambo la kuoa,wazazi walilijua,
sisi twajiamulia,wachumba jichagulia,
kule kwao hujajua,uchumba jitangazia,
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka.
Huyo mke ulooa,wala kwao hupajui,
naye aliyekuoa,kesho atakukinai,
sababu usije zua,mila zao huzijui,
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka
Magonjwa unayajua,kutaja yote siwezi,
zipo koo za vichaa,zingine za wadokozi,
lipi unaloshangaa,wengine ni wachochezi
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka.
Lugha ile ya mafumbo,wazee walitumia,
hawakutumia fimbo,ujumbe kutupatia,
sasa vya nini vikumbo,tulia fuatilia,
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka
Kwa mama wajawazito,kula mayai ni mwiko,
huu ulikuwa wito,kumbuka sayansi yako,
usiwaze kwa mkato,ulikuwa kweli mwiko,
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka.
Zikumbuke enzi hizo,hospitali za shida,
kujifungua tatizo,tena kwachukua muda,
toto linene katizo,hili jibu sio mada,
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka.
Hebu fanya uchunguzi,ndoa zile za zamani,
hawakuwa wapuuzi,wala ndani tafrani,
hizi ndoa siku hizi,ni kama tuko vitani
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka.
Watoto wako wavivu,nini unachoshangaa,
umeshalipata kovu,katu huwezi litoa,
hata kama kwa mabavu,umeshaingia doa,
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka
Beti kumi zinatosha,sasa nikapumzike,
hata kama zinachusha,ziweke mahali pake,
usasa umenichosha,ndoa zetu sekeseke
Nyingi si mila potofu,ni sisi tunapotoka.
NYUMBA YA AJABU
Jambo hili lashangaza,kuanza kusimulia,
kutwa kucha ninawaza,niweze kuhadithia,
jambo hili lanikwaza,akili kutotulia,
Kuishi ni kazi ngumu,mume na mke pamoja.
Mama anapokosea,hebu muite chumbani,
fidhuli wamletea,kubwatuka sebuleni,
busara ikitopea,nyumba yenu itawini,
Kuishi ni kazi ngumu,mume na mke pamoja.
Mama anapokosea,wawaeleza watoto,
hekima imepungua,mambo ya mkato,
busara imepungua,mambo mfano pilato,
Kuishi ni kazi ngumu,mume na mke pamoja
Mama kosa amefanya,umekwisha kasirika,
lini ulipomuonya,unaanza kubwatuka,
hata kama wamkanya,ameanza kirihika,
Kuishi ni kazi ngumu,mume na mke pamoja
Mke nawe washangaza,linapotokea jambo,
unaanza kutangaza,na pengine kwa mafumbo,
sasa watakupuuza,yapunguze majigambo,
Kuishi ni kazi ngumu,mume na mke pamoja
kutwa kucha ninawaza,niweze kuhadithia,
jambo hili lanikwaza,akili kutotulia,
Kuishi ni kazi ngumu,mume na mke pamoja.
Mama anapokosea,hebu muite chumbani,
fidhuli wamletea,kubwatuka sebuleni,
busara ikitopea,nyumba yenu itawini,
Kuishi ni kazi ngumu,mume na mke pamoja.
Mama anapokosea,wawaeleza watoto,
hekima imepungua,mambo ya mkato,
busara imepungua,mambo mfano pilato,
Kuishi ni kazi ngumu,mume na mke pamoja
Mama kosa amefanya,umekwisha kasirika,
lini ulipomuonya,unaanza kubwatuka,
hata kama wamkanya,ameanza kirihika,
Kuishi ni kazi ngumu,mume na mke pamoja
Mke nawe washangaza,linapotokea jambo,
unaanza kutangaza,na pengine kwa mafumbo,
sasa watakupuuza,yapunguze majigambo,
Kuishi ni kazi ngumu,mume na mke pamoja
NANI ATAKUTAFUTA
Mara nyingi nashangaa,kwa mambo ya walimwengu,
visa wanavyovizua,vinanitia uchungu,
majibu wanayotoa,yazua kizunguzungu,
Nani atakutafuta,kama wewe ni fukara.
Kumbuka ulipofiwa,nani alikufuata,
ulibakia mkiwa,machozi kufutafuta,
hakuna ulichopewa,hata kande hukupata,
Nani atakutafuta,kama wewe ni fukara.
Kumbuka harusi yako,watu walivyokususa,
suti kama mbwa koko,au muuza msusa,
shela nalo ni kicheko,kama hukutoa pesa,
Nani atakutafuta,kama wewe ni fukara.
Kilio kimetokea,wewe hawakujulishi,
nini utajitolea,wanakuona mzushi,
machozi unayatoa,kwao sawa na bileshi,
Nani atakutafuta,kama wewe ni fukara.
Busara kweli unayo,lakini pesa hauna,
hoja nzito utoayo,uzito kweli haina,
kazi yako ni miayo,kipara unakikuna,
Nani atakutafuta, kama wewe ni fukara.
Kaka yako wa Kigoma,yeye anako kagari,
mdogo kule Dodoma,ana boma la fahari,
mdogo wako Satima,ana shamba la shayiri
Nani atakutafuta,kama wewe ni fukara
visa wanavyovizua,vinanitia uchungu,
majibu wanayotoa,yazua kizunguzungu,
Nani atakutafuta,kama wewe ni fukara.
Kumbuka ulipofiwa,nani alikufuata,
ulibakia mkiwa,machozi kufutafuta,
hakuna ulichopewa,hata kande hukupata,
Nani atakutafuta,kama wewe ni fukara.
Kumbuka harusi yako,watu walivyokususa,
suti kama mbwa koko,au muuza msusa,
shela nalo ni kicheko,kama hukutoa pesa,
Nani atakutafuta,kama wewe ni fukara.
Kilio kimetokea,wewe hawakujulishi,
nini utajitolea,wanakuona mzushi,
machozi unayatoa,kwao sawa na bileshi,
Nani atakutafuta,kama wewe ni fukara.
Busara kweli unayo,lakini pesa hauna,
hoja nzito utoayo,uzito kweli haina,
kazi yako ni miayo,kipara unakikuna,
Nani atakutafuta, kama wewe ni fukara.
Kaka yako wa Kigoma,yeye anako kagari,
mdogo kule Dodoma,ana boma la fahari,
mdogo wako Satima,ana shamba la shayiri
Nani atakutafuta,kama wewe ni fukara
Monday, September 5, 2011
NDOA ZETU
Ndoa zetu siku hizi,ni kama tuko vitani,
ni rahisi kumaizi,vita huko majumbani,
huna haja kubarizi,ukweli kuubaini,
Ninazitamani ndoa,zile za mababu zetu.
Zimejaa fumanizi,ndoa kama ni utani,
nyingi ni za kipuuzi,linaniuma moyoni,
afadhali kikohozi,dawa hospitalini,
Ninazitamani ndoa,zile za mababu zetu.
Zilithamini makuzi,kweli nasema jamani,
koo zile zenye wezi,kuoa singetamani,
ndoa pasipo ujuzi,nani angezithamini,
Ninazitamani ndoa,zile za mababu zetu.
Sasa ndoa ni mapozi,yote haya naamini,
kama sio makohozi,ulotema mdomoni,
wote huu ni uchizi,linaniuma moyoni,
Ninazitamani ndoa,zile za mababu zetu.
Ndoa hii mwaka juzi,leo haina thamani,
nyumba sasa si makazi,ndani kutwa tafrani,
nani kwenu mchokozi,kasuluhisheni ndani,
Ninazitamani ndoa,zile za mababu zetu.
Ndoa sio mazoezi,kujaribu uwanjani,
likitokea dowezi,kwa mbali lifukuzeni,
muuache ubazazi,rudini ndani chumbani,
Ninazitamani ndoa,zile za mababu zetu.
Ndoa hizi siku hizi,hazimjui Manani,
kwa waganga kama kazi,hiyo kwenu kwenu ndio fani
Muumba hatumjuzi,tukigombana nyumbani,
Ninazitamani ndoa,zile za mababu zetu.
Namaliza kubarizi,ondokeni mkumboni,
msitumie hirizi,hamtodumu ndoani,
ndoa hizi za mizizi,jibu lake kaburini
Ninazitamani ndoa,zile za mababu zetu.
ni rahisi kumaizi,vita huko majumbani,
huna haja kubarizi,ukweli kuubaini,
Ninazitamani ndoa,zile za mababu zetu.
Zimejaa fumanizi,ndoa kama ni utani,
nyingi ni za kipuuzi,linaniuma moyoni,
afadhali kikohozi,dawa hospitalini,
Ninazitamani ndoa,zile za mababu zetu.
Zilithamini makuzi,kweli nasema jamani,
koo zile zenye wezi,kuoa singetamani,
ndoa pasipo ujuzi,nani angezithamini,
Ninazitamani ndoa,zile za mababu zetu.
Sasa ndoa ni mapozi,yote haya naamini,
kama sio makohozi,ulotema mdomoni,
wote huu ni uchizi,linaniuma moyoni,
Ninazitamani ndoa,zile za mababu zetu.
Ndoa hii mwaka juzi,leo haina thamani,
nyumba sasa si makazi,ndani kutwa tafrani,
nani kwenu mchokozi,kasuluhisheni ndani,
Ninazitamani ndoa,zile za mababu zetu.
Ndoa sio mazoezi,kujaribu uwanjani,
likitokea dowezi,kwa mbali lifukuzeni,
muuache ubazazi,rudini ndani chumbani,
Ninazitamani ndoa,zile za mababu zetu.
Ndoa hizi siku hizi,hazimjui Manani,
kwa waganga kama kazi,hiyo kwenu kwenu ndio fani
Muumba hatumjuzi,tukigombana nyumbani,
Ninazitamani ndoa,zile za mababu zetu.
Namaliza kubarizi,ondokeni mkumboni,
msitumie hirizi,hamtodumu ndoani,
ndoa hizi za mizizi,jibu lake kaburini
Ninazitamani ndoa,zile za mababu zetu.
Friday, September 2, 2011
CHAKULA CHAKO WAKILA,HATA CHA MTOTO PIA!
Baba unanishangaza,unavyopenda chakula,
hakuna haja kuwaza,wala kumuomba Mola,
watoto unatukwaza,sasa twaanzisha vita,
Chakula chako wakila,hata cha watoto pia
Watoto tukale wapi,ukila chakula chetu
watudanganya kwa pipi,pipi sio mila kwetu,
akili zetu si fupi,kutufanya ni vibutu,
Chakula chako wakila,hata cha watoto pia
watoto twakushangaa,unavyodoea vyetu
chakula unanunua,tena kile cha kikwetu,
vipi tena wachukua,hatupendi hiyo katu
Chakula chako wakila,hata cha watoto pia.
Shilingi mia kwa nini,wagombea na mtoto,
unapata milioni,tena njia za mkato,
kwa mtoto kuna nini,mambo yake batobato,
Chakula chako wakila,hata cha mtoto pia.
Babu kaleta zawadi,nawe macho juu juu,
sijaiona abadi,tabia ya kijukuu,
kusema mi sina budi,sijepalia kifuu,
Chakula chako wakila,hata cha mtoto pia.
Kile kilicho cha kwako,watoto hatukigusi,
vilivyo sirini mwako,waficha kama fukusi,
tunajua nia yako,mbaya mfano wa fisi,
Chakula chako wakila,hata cha mtoto pia.
Nilipopewa mkate,wewe uliutamani,
ulianza meza mate,ukawaza akilini,
vipi ukaukamate,ukaufiche chumbani,
Chakula chako wakila,hata cha watoto pia.
Vyakula vyako ni vingi,sote tunavibaini,
hatuviweki vigingi,wenda kula hotelini,
waweka gani misingi,tuliobaki nyumbani
Chakula chako wakila,hata cha watoto pia.
hakuna haja kuwaza,wala kumuomba Mola,
watoto unatukwaza,sasa twaanzisha vita,
Chakula chako wakila,hata cha watoto pia
Watoto tukale wapi,ukila chakula chetu
watudanganya kwa pipi,pipi sio mila kwetu,
akili zetu si fupi,kutufanya ni vibutu,
Chakula chako wakila,hata cha watoto pia
watoto twakushangaa,unavyodoea vyetu
chakula unanunua,tena kile cha kikwetu,
vipi tena wachukua,hatupendi hiyo katu
Chakula chako wakila,hata cha watoto pia.
Shilingi mia kwa nini,wagombea na mtoto,
unapata milioni,tena njia za mkato,
kwa mtoto kuna nini,mambo yake batobato,
Chakula chako wakila,hata cha mtoto pia.
Babu kaleta zawadi,nawe macho juu juu,
sijaiona abadi,tabia ya kijukuu,
kusema mi sina budi,sijepalia kifuu,
Chakula chako wakila,hata cha mtoto pia.
Kile kilicho cha kwako,watoto hatukigusi,
vilivyo sirini mwako,waficha kama fukusi,
tunajua nia yako,mbaya mfano wa fisi,
Chakula chako wakila,hata cha mtoto pia.
Nilipopewa mkate,wewe uliutamani,
ulianza meza mate,ukawaza akilini,
vipi ukaukamate,ukaufiche chumbani,
Chakula chako wakila,hata cha watoto pia.
Vyakula vyako ni vingi,sote tunavibaini,
hatuviweki vigingi,wenda kula hotelini,
waweka gani misingi,tuliobaki nyumbani
Chakula chako wakila,hata cha watoto pia.
USIWAIGE WAVUVI
Ziwani samaki wengi,wa aina mbalimbali,
wavuvi waona mengi,waweza usikubali
mitego mingi watega,mingine kwenye jabali,
Wavuvi kazi wanayo,katu huwezi waiga
Wavuvi mahala pengi,hawavai suruali,
hawaibebi mitungi,bali wana vibakuli,
mitego watega mingi,mingine kwenye jabali,
. Wavuvi kazi wanayo,katu huwezi waiga
Tembelea baharini,au wale wa ziwani,
kawaone wa mitoni,au kule mabwawani,
tofauti huioni,muda mwingi ni majini,
Wavuvi kazi wanayo,katu huwezi waiga
Samaki aina nyingi,kuwapata ni adimu,
pweza ana visa vingi,aweza kutoa damu,
mbasa kwenye kina kingi,kumpata ni adimu,
Wavuvi kazi wanayo,katu huwezi waiga.
Samaki niliyepata,wavuvi wanashangaa,
kozi hiyo sijapata ya kuingia kuvua,
samaki niliyepata,wote macho watumbua
Wavuvi kazi wanayo,katu huwezi waiga
Nilipotupa ndoano,mshipi akaukata,
kitu nilichokiona,hasira ikanipata,
sikupenda kushindana,ujasiri nikapata,
Wavuvi kazi wanayo,katu siwezi waiga.
Nikalitupa jarife,hili sasa litafaa,
hata ikibidi nife,samaki nitamvua,
hatalikata jarife,hivi nimeshamvua,
Wavuvi kazi wanayo,katu siwezi waiga.
Samaki niliyevua,nitamtunza chumbani,
wengi mtanishangaa,simuweki sebuleni,
huyu kweli si dagaa,nimuanike juani,
Wavuvi kazi wanayo,katu siwezi waiga.
Samaki kanisumbua,kutwa kucha kumtega,
kitu nilichogundua,hamkujua kutega,
muda ulipotimia,mtego hakuumega,
Wavuvi kazi wanayo,katu siwezi waiga
Samaki ni mali yangu,sitogawana na mtu,.
namweka chumbani mwangu,katu hutoona kitu,
nitamfumbata mwangu,wamwone wazazi wetu,
Wavuvi kazi wanayo,katu siwezi waiga.
wavuvi waona mengi,waweza usikubali
mitego mingi watega,mingine kwenye jabali,
Wavuvi kazi wanayo,katu huwezi waiga
Wavuvi mahala pengi,hawavai suruali,
hawaibebi mitungi,bali wana vibakuli,
mitego watega mingi,mingine kwenye jabali,
. Wavuvi kazi wanayo,katu huwezi waiga
Tembelea baharini,au wale wa ziwani,
kawaone wa mitoni,au kule mabwawani,
tofauti huioni,muda mwingi ni majini,
Wavuvi kazi wanayo,katu huwezi waiga
Samaki aina nyingi,kuwapata ni adimu,
pweza ana visa vingi,aweza kutoa damu,
mbasa kwenye kina kingi,kumpata ni adimu,
Wavuvi kazi wanayo,katu huwezi waiga.
Samaki niliyepata,wavuvi wanashangaa,
kozi hiyo sijapata ya kuingia kuvua,
samaki niliyepata,wote macho watumbua
Wavuvi kazi wanayo,katu huwezi waiga
Nilipotupa ndoano,mshipi akaukata,
kitu nilichokiona,hasira ikanipata,
sikupenda kushindana,ujasiri nikapata,
Wavuvi kazi wanayo,katu siwezi waiga.
Nikalitupa jarife,hili sasa litafaa,
hata ikibidi nife,samaki nitamvua,
hatalikata jarife,hivi nimeshamvua,
Wavuvi kazi wanayo,katu siwezi waiga.
Samaki niliyevua,nitamtunza chumbani,
wengi mtanishangaa,simuweki sebuleni,
huyu kweli si dagaa,nimuanike juani,
Wavuvi kazi wanayo,katu siwezi waiga.
Samaki kanisumbua,kutwa kucha kumtega,
kitu nilichogundua,hamkujua kutega,
muda ulipotimia,mtego hakuumega,
Wavuvi kazi wanayo,katu siwezi waiga
Samaki ni mali yangu,sitogawana na mtu,.
namweka chumbani mwangu,katu hutoona kitu,
nitamfumbata mwangu,wamwone wazazi wetu,
Wavuvi kazi wanayo,katu siwezi waiga.
KAZI WALISTAAFU TENA MNAWAPA KAZI.
Nimejiuliza sana,wapi tunaelekea
kichwani ninajikuna,jibu kujitafutia
wakubwa wanatubana,haki yote yapotea,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Watoto twawasomesha,pesa nyingi tunalipa,
kutwa kucha walikesha,ile elimu kupata,
sasa mnawazungusha,tena sasa mwawatupa,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Nisemayo si majungu,ni jambo la uhakika,
imenitia uchungu,wanyonge twasikitika,
hata kule kwa wazungu ,jambo hili limefika,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi
Hebu jaribu chunguza,haya ninayoyasema,
lakini kasi punguza,kazi yako iwe njema,
usije lengo poteza,ukabaki na kilema,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Udugu umeshamiri,ingawa tunaukana,
urafiki ni mahiri,wewe kando utabana
kazi sasa sio siri,mambo yote kujuana,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Mwasema ni wazoefu,ndio mana wanarudi,
yatia kichefuchefu,kusema sinayo budi,
sio maneno machafu,mimi nasema abadi,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Waliotoka shuleni,kazi waipate wapi?
mmejaa ofisini,wao wakauze pipi,
rejeeni vijijini,mmekuwa fotokopi,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Mtoto wa mkulima,ataishia kulima,
na hata akijituma,hapo kwenye taaluma,
mambo yalivyo mrama,ataishia lalama,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Elimu utayosoma,ikusaidie wewe,
usianze kuzozoma,ukajitia kiwewe
ninakukata kalima,kazi hizo za wenyewe
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Mliopo makazini,kazi yenu ithamini,
wakiletwa ofisini,jamani wapokeeni,
lakini muwe makini,msingie matatani,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Beti hizo zinatosha,kama ukizingatia,
sio lengo kuwachosha,dukuduku nimetoa,
pumzi sasa nashusha,moyo unachekelea
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
kichwani ninajikuna,jibu kujitafutia
wakubwa wanatubana,haki yote yapotea,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Watoto twawasomesha,pesa nyingi tunalipa,
kutwa kucha walikesha,ile elimu kupata,
sasa mnawazungusha,tena sasa mwawatupa,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Nisemayo si majungu,ni jambo la uhakika,
imenitia uchungu,wanyonge twasikitika,
hata kule kwa wazungu ,jambo hili limefika,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi
Hebu jaribu chunguza,haya ninayoyasema,
lakini kasi punguza,kazi yako iwe njema,
usije lengo poteza,ukabaki na kilema,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Udugu umeshamiri,ingawa tunaukana,
urafiki ni mahiri,wewe kando utabana
kazi sasa sio siri,mambo yote kujuana,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Mwasema ni wazoefu,ndio mana wanarudi,
yatia kichefuchefu,kusema sinayo budi,
sio maneno machafu,mimi nasema abadi,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Waliotoka shuleni,kazi waipate wapi?
mmejaa ofisini,wao wakauze pipi,
rejeeni vijijini,mmekuwa fotokopi,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Mtoto wa mkulima,ataishia kulima,
na hata akijituma,hapo kwenye taaluma,
mambo yalivyo mrama,ataishia lalama,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Elimu utayosoma,ikusaidie wewe,
usianze kuzozoma,ukajitia kiwewe
ninakukata kalima,kazi hizo za wenyewe
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Mliopo makazini,kazi yenu ithamini,
wakiletwa ofisini,jamani wapokeeni,
lakini muwe makini,msingie matatani,
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
Beti hizo zinatosha,kama ukizingatia,
sio lengo kuwachosha,dukuduku nimetoa,
pumzi sasa nashusha,moyo unachekelea
Kazi walistaafu,tena mnawapa kazi.
KAZI NI KUPATA KAZI
Kichwani lanitatiza,swali lihusulo kazi,
kutwa kucha ninawaza,sijapata ufumbuzi,
majibu mengi nawaza,yote hayatoshelezi,
Kweli huu ni ukweli,kazi ni kupata kazi.
Nilipokuwa shuleni,sana nilijiliwaza,
mitihani nikiwini,sana nitajiliwaza,
sikuwaza akilini,mambo yatanitatiza,
Kweli huu ni ukweli,kazi in kupata kazi.
Nilipotafuta kazi,sana nilihangaika,
watu kunishuku wizi,kwa nilivyosakasaka,
rushwa kuiomba wazi,ofisini nikifika,
Kweli huu ni ukweli,kazi ni kupata kazi.
Kazi nilipoipata,moyo ukanitulia
mapesa nitasakata,vijiweni watalia,
kumbe bado ni ukata,vibaya kusimulia,
Kweli huu ni ukweli,kazi ni kupata kazi
Mshahara wasumbua,sivyo nilivyodhania,
sasa kilichobakia,siku kuzihesabia,
nashindwa kutegemea,lini watanipatia,
Kweli huu ni ukweli,kazi ni kupata kazi..
kutwa kucha ninawaza,sijapata ufumbuzi,
majibu mengi nawaza,yote hayatoshelezi,
Kweli huu ni ukweli,kazi ni kupata kazi.
Nilipokuwa shuleni,sana nilijiliwaza,
mitihani nikiwini,sana nitajiliwaza,
sikuwaza akilini,mambo yatanitatiza,
Kweli huu ni ukweli,kazi in kupata kazi.
Nilipotafuta kazi,sana nilihangaika,
watu kunishuku wizi,kwa nilivyosakasaka,
rushwa kuiomba wazi,ofisini nikifika,
Kweli huu ni ukweli,kazi ni kupata kazi.
Kazi nilipoipata,moyo ukanitulia
mapesa nitasakata,vijiweni watalia,
kumbe bado ni ukata,vibaya kusimulia,
Kweli huu ni ukweli,kazi ni kupata kazi
Mshahara wasumbua,sivyo nilivyodhania,
sasa kilichobakia,siku kuzihesabia,
nashindwa kutegemea,lini watanipatia,
Kweli huu ni ukweli,kazi ni kupata kazi..
Thursday, September 1, 2011
HATA MIMI NASHANGAA.
Jinsi unavyoshangaa,hata mimi nashangaa,
jambo lililotokea,kweli ni kizaaza,
sitoweza vumilia,kichwa kipate tulia,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa
Habari ilozagaa,akili bado tulia,
eti mtoto kuzaa,na baba alomzaa,
kamwe mi sitotulia,sipati huo wasaa,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa.
Mama binti wagombea,'kabuzi'kalobobea,
mimacho wametumbua,kijana wagombania,
wote ni viruka njia,ukimwi jitafutia,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa
Mwalimu na mwanafunzi,eti nao ni wapenzi,
haya ni gani mafunzi,huu kwetu ni ushenzi,
natamani piga konzi,au kibao cha banzi,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa.
Baba na mtoto wako,mnachangia kimada,
ninyi sawa mbwa koko,kuzurura kwake ada,
kama ni wali ukoko,hamfai kwenye eda,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa.
Dakitari wanichosha,mgonjwa wamtamani,
nani alikufundisha,sijaona asilani,
badala kumponesha,mapenzi wamtamani,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa.
Wewe bosi ofisini,hakika watia fora,
umuonapo karani,moyoni wapiga kura,
fikiria akilini,uhai ni kitu bora,
Hata mimi nashangaa jinsi unavyoshangaa.
Ewe kabinti kadogo,uhai kwako ni mali,
watembea kwa mikogo,kupita kila mahali,
kwa rika bado mdogo,bado kukua akili,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa.
Na viongozi wa dini,pepo huyo awatoke,
mwatamani waumini,mwalizua sekeseke,
hili utalibaini waulize wanawake,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa.
Nani aliyebakia,MOLA akajivunia,
utukufu tumevua,tumevaa magunia,
wangapi wamesalia,Mungu kuwahurumia,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa..
,
jambo lililotokea,kweli ni kizaaza,
sitoweza vumilia,kichwa kipate tulia,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa
Habari ilozagaa,akili bado tulia,
eti mtoto kuzaa,na baba alomzaa,
kamwe mi sitotulia,sipati huo wasaa,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa.
Mama binti wagombea,'kabuzi'kalobobea,
mimacho wametumbua,kijana wagombania,
wote ni viruka njia,ukimwi jitafutia,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa
Mwalimu na mwanafunzi,eti nao ni wapenzi,
haya ni gani mafunzi,huu kwetu ni ushenzi,
natamani piga konzi,au kibao cha banzi,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa.
Baba na mtoto wako,mnachangia kimada,
ninyi sawa mbwa koko,kuzurura kwake ada,
kama ni wali ukoko,hamfai kwenye eda,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa.
Dakitari wanichosha,mgonjwa wamtamani,
nani alikufundisha,sijaona asilani,
badala kumponesha,mapenzi wamtamani,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa.
Wewe bosi ofisini,hakika watia fora,
umuonapo karani,moyoni wapiga kura,
fikiria akilini,uhai ni kitu bora,
Hata mimi nashangaa jinsi unavyoshangaa.
Ewe kabinti kadogo,uhai kwako ni mali,
watembea kwa mikogo,kupita kila mahali,
kwa rika bado mdogo,bado kukua akili,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa.
Na viongozi wa dini,pepo huyo awatoke,
mwatamani waumini,mwalizua sekeseke,
hili utalibaini waulize wanawake,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa.
Nani aliyebakia,MOLA akajivunia,
utukufu tumevua,tumevaa magunia,
wangapi wamesalia,Mungu kuwahurumia,
Hata mimi nashangaa,jinsi unavyoshangaa..
,
Thursday, August 25, 2011
MHESHIMIWA NI NANI?
Rais mheshimiwa,Makamu mheshimiwa
waziri mheshimiwa,naibu mheshimiwa,
spika mheshimiwa,katibu mheshimiwa,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Mimi ni mkata miwa,hivi si mheshimiwa?
kutwa nakatwa na miwa,pesa kichele napewa,
na hao waheshimiwa ,kila kitu wanapewa
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?,
Hakimu mheshimiwa,wakili mheshimiwa,
wada ni mheshimiwa,afande mheshimiwa,
diwani mheshimiwa,balozi mheshimiwa,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Mhudumu ofisini,siitwi mheshimiwa,
mpika chai shuleni,siitwi mheshimiwa,
msafishaji chooni,siitwi mheshimiwa,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Padri mheshimiwa,Shehe ni mheshimiwa,
mbunge mheshimiwa,mjumbe mheshimiwa,
tajiri mheshimiwa,fukara alaumiwa,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Mimi nalima shambani,siitwi mheshimiwa,
navuta mkokoteni,siitwi mheshimiwa,
nesi hospitalini,siitwi,mheshimiwa,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Huyu mkuu wa shule,aitwa mheshimiwa,
rafiki badi Bakule,haitwi mheshimiwa,
bwana kaka kando kule,wewe ni mheshimiwa,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Mgonjwa hospitali,haitwi mheshimiwa,
mwenye nzuri yake hali,haitwi mheshimiwa,
mwenye kuchunga fahali,haitwi mheshimiwa,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Mambo mnayaharibu,eti ni waheshimiwa,
mnajitia mabubu,maswali mkitupiwa,
matatizo yatusibu,porojo zenu twalewa,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Konisaga nashangaa,wapi tunaelekea,
neno ndugu lapotea,gizani latokomea,
hakika tulizoea,udugu liliulea,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Sasa ninamalizia,neno hilo silipendi,
sana laleta udhia,latuletea makundi
usawa utapotea,sawa wa njiwa na bundi,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
,
waziri mheshimiwa,naibu mheshimiwa,
spika mheshimiwa,katibu mheshimiwa,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Mimi ni mkata miwa,hivi si mheshimiwa?
kutwa nakatwa na miwa,pesa kichele napewa,
na hao waheshimiwa ,kila kitu wanapewa
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?,
Hakimu mheshimiwa,wakili mheshimiwa,
wada ni mheshimiwa,afande mheshimiwa,
diwani mheshimiwa,balozi mheshimiwa,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Mhudumu ofisini,siitwi mheshimiwa,
mpika chai shuleni,siitwi mheshimiwa,
msafishaji chooni,siitwi mheshimiwa,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Padri mheshimiwa,Shehe ni mheshimiwa,
mbunge mheshimiwa,mjumbe mheshimiwa,
tajiri mheshimiwa,fukara alaumiwa,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Mimi nalima shambani,siitwi mheshimiwa,
navuta mkokoteni,siitwi mheshimiwa,
nesi hospitalini,siitwi,mheshimiwa,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Huyu mkuu wa shule,aitwa mheshimiwa,
rafiki badi Bakule,haitwi mheshimiwa,
bwana kaka kando kule,wewe ni mheshimiwa,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Mgonjwa hospitali,haitwi mheshimiwa,
mwenye nzuri yake hali,haitwi mheshimiwa,
mwenye kuchunga fahali,haitwi mheshimiwa,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Mambo mnayaharibu,eti ni waheshimiwa,
mnajitia mabubu,maswali mkitupiwa,
matatizo yatusibu,porojo zenu twalewa,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Konisaga nashangaa,wapi tunaelekea,
neno ndugu lapotea,gizani latokomea,
hakika tulizoea,udugu liliulea,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
Sasa ninamalizia,neno hilo silipendi,
sana laleta udhia,latuletea makundi
usawa utapotea,sawa wa njiwa na bundi,
Hili linanichanganya,nani ni mheshimiwa?
,
Wednesday, August 24, 2011
SWALA TUMETEGA WOTE
Tu wawindaji pamoja,porini tumeingia,
sote tumejenga hoja,wanyama kujipatia,
hata sungura akija,sawa tutajigawia,
Swala tumetega wote,vipi ule peke yako?
windoni tulipotega,macho tukayapanua,
walisogolea mbega,balaa kutuletea,
tukajifunga lubega,mbali kuwafukuzia,
Swala tumetegaa wote vipi ule peke yako?
Twajua wewe mkubwa,kati yetu wawindaji,
hata kuwinda kwa mbwa,kelele utahitaji,
huwezi ruka kwa mbwa,hunacho hicho kipaji,
Swala tumetega wote,vipi ule peke yako?
Tulipoanza usasi,umoja tuliujenga,
hatukuwa na risasi,marungu tuliyatenga,
hakutokea muasi,kati kulileta janga,
Swala tumetega wote,vipi ule peke yako?
Tulijipangia zamu,kwenda kuona mitego,
tena kwa mashamushamu,tulikwenda kwa mikogo,
nasi hatukufahamu,kumbe kuna mikorogo,
Swala tumetega wote,vipi ule peke yako?
Swala alipotegeka,ilikuwa zamu yako,
begani ukamuweka,haraka chumbani kwako,
chini ukajibweteka,umezua sokomoko,
Swala tumetega wote,vipi ule peke yako?
Msiri ulomwambia,yeye hajui kuchuna,
kisu atakupatia,swala mpate kuchuna,
uchoyo umekujia,hasidi lako ni jina,
Swala tumetega wote,vipi ule peke yako?
sote tumejenga hoja,wanyama kujipatia,
hata sungura akija,sawa tutajigawia,
Swala tumetega wote,vipi ule peke yako?
windoni tulipotega,macho tukayapanua,
walisogolea mbega,balaa kutuletea,
tukajifunga lubega,mbali kuwafukuzia,
Swala tumetegaa wote vipi ule peke yako?
Twajua wewe mkubwa,kati yetu wawindaji,
hata kuwinda kwa mbwa,kelele utahitaji,
huwezi ruka kwa mbwa,hunacho hicho kipaji,
Swala tumetega wote,vipi ule peke yako?
Tulipoanza usasi,umoja tuliujenga,
hatukuwa na risasi,marungu tuliyatenga,
hakutokea muasi,kati kulileta janga,
Swala tumetega wote,vipi ule peke yako?
Tulijipangia zamu,kwenda kuona mitego,
tena kwa mashamushamu,tulikwenda kwa mikogo,
nasi hatukufahamu,kumbe kuna mikorogo,
Swala tumetega wote,vipi ule peke yako?
Swala alipotegeka,ilikuwa zamu yako,
begani ukamuweka,haraka chumbani kwako,
chini ukajibweteka,umezua sokomoko,
Swala tumetega wote,vipi ule peke yako?
Msiri ulomwambia,yeye hajui kuchuna,
kisu atakupatia,swala mpate kuchuna,
uchoyo umekujia,hasidi lako ni jina,
Swala tumetega wote,vipi ule peke yako?
Tuesday, August 23, 2011
KIFUNGUA MACHO
SHAIRI LA SALAMU.
Uanze kwa kufikiri,unapotunga shairi,
kuyapanga mashairi,yapasa uwe mahiri,
kuifikisha habari,ni kazi kweli si siri,
Hatutaki ufahari,ushairi ni safari.
Uanze kwa kufikiri,unapotunga shairi,
kuyapanga mashairi,yapasa uwe mahiri,
kuifikisha habari,ni kazi kweli si siri,
Hatutaki ufahari,ushairi ni safari.
Subscribe to:
Posts (Atom)